Monday, April 6, 2009

UBALOZI WA RWANDA KUCHANGISHA FEDHA KUSAIDIA YATIMA WA MAUAJI YA KIMBARI YA MWAKA 1994

Balozi wa Rwanda Nchini Zeno Mutimura akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari maelezo leo juu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini humo mwaka 1994 miaka 15 iliyopita yanayotarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Karimjee jijini
Nakaaya Sumari akielezea wandishi wa habari juu ya wimbo wake wa I am in Africa alioutunga maalum kwa ajili ya kampeni ya kusaidia yatima waliotokana na mauaji ya kimbari mwaka 1994 nchini Rwanda ubalozi wa Rwanda na umoja wa mataifa wataadhimisha kukumbuka mauaji hayo kesho kwenye ukumbi wa Karimjee jijini.

Kutoka kulia ni wanamuziki Enika Bukuku, Chid Benz, Nakaaya Sumari na Sauda Simba Nakaaya ametunga wimbo unaoitwa I am in Africa unaowaonya waafrika kutothubutu kufanya mambo ambayo yanaweza kupelekea mauaji ya Kimbari kama yaliyotokea nchini Rwanda miaka 15 iliyopita lakini pia kuhamasisha waafrika wakiwemo Tanzania kuchangia japo dola moja tu kwa ajili ya kusaidia yatima waliopoteza wazazi kutokana na mauaji


Balozi wa Rwanda Nchini Zeno Mutimura alizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari maelezo leo juu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini humo mwaka 1994 miaka 15 iliyopita yanayotarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam
Katika maadhimisho hayo pia kutakuwa na wimbo maalum uliotungwa na mwanamuziki Nakaaya Sumari unaoitwa I am in Africa kuachana na mambo ambayo yanaweza kuchochea kwa mauaji kama yaliyotokea Rwanda laakini pia unaozungumzia kampeni ya kuwasaidia yatima walioko nchini Rwanda waliopoteza wazazi kutokana na mauaji hayo watu mbalimbali na mashirika wameombwa kuchangia kuazia dola moja na kuendelea.
Balozi Mutimura amezitaja akaunti zitakazotumika kukusanya michango hiyo kuwa ni National Bank of Commerce Emassy of Rwanda Acc No. USD:012105025668 na Acc no: Tsh: 012103016937 kampeni hii itaendeshwa kwa muda wa siku 100 ili kukusanya michango hii katika picha kushoto ni Usia Nkhoma afisa habari wa umoja wa mataifa.
Msomaji
Dar es salaam

No comments: