Thursday, April 2, 2009

MELI YAKWAMA KWENYE BANDARI YA SALAMA

Hii ndio meli iliyokwama bandari pale Dar es salaam baada ya kupoteza mwelekeo. Meli hii inaitwa MSC Federica.
Jinsi Meli ilivyokwama kwenye mchanga.
Katibu Mkuu wa wizara ya Miundombinu Omar Chambo akiongea na waandishi wa habari kuhusu kukwama kwa meli hiyo ya mizigo katika eneo la Feri ya Kigamboni baada ya kutokea matatizo kwenye usukani na kushindwa kukata kona, meli ilikuwa inatokea katika Bandari ya Dar es Salaam kuelekea nchi za nje. Juhudi za kuikwamua zinaendelea ikiwa ni pamoja na kupunguza maji na mafuta kwenye meli ili kupunguza uzito
Katibu Mkuu akiangalia meli hiyo ya MSC Federica katika eneo la Feri ya Kigamboni Habour Master nahodha Juma Saire akimuonyesha Katibu Mkuu wa wizara ya Miundombinu Omar Chambo (katikati) meli hiyo ya MSC Federica iliyokwama bandalini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa bandari Ephraim Mgawe.
MSC Federica kwa mbali kutokea maeneo ya Feri ya Kigamboni . Juhudi za kuikwamua zinaendelea ikiwa ni pamoja na kupunguza maji na mafuta kwenye meli ili kupunguza uzito.

Msomaji
Dar es salaam

No comments: