Thursday, April 2, 2009

SIKU MH CHENGE ALIPOTA AJALI MBAYA NA KUUA WATU WAWILI.

Mbunge wa CCM wa jimbo la Bariadi Mashariki , Mh, Andrew Chenge alipata ajali ya gari alilokuwa akiendesha aina ya Totota Hillux lenye namba za usajili T512ACE katika maeneo ya makutano ya barabara za Haillesalasie na Karume eneo la Oysterbay jijini na kuua watu wawili papoapo.
Gari la Mh Chenge liligonga Bajaji yenye namba za usajili T736AHC na kusababisha vifo vya watu wawili ambao walikuwa abiria katika bajaj hiyo.
Chenge akiwa Polisi Oysterbay.
Mh Chenge akiwa katika eneo la ajali.
Askari Polisi wa traffic akibeba baadhi ya mabaki yaliochwa kwenye ajali.
Mh Chenge akiwapungia watoto wa shule mkono kana kwamba alienda kufanya ziara.
Hata baadhi ya maafande pia walianza kupungia mikono watoto.
Msomaji
Dar es salaam

No comments: