Thursday, August 20, 2009

KONGAMANO LA KUJADILI ATHARI ZA UANDIKISHWAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA PEMBA LAENDELEA JIJINI!

Wanasiasa Mashuhuri nchini wakielekea kwenye ukumbi wa mkutano mara baada ya mapumziko mafupi katika kongamano la kujadili Athari za Uandikishaji wa Daftari la Wapiga Kura Kisiwani Pemba lililofanyika Karimjee Hall.

Viongozi na wadau mabalimabli wa siasa wakiwemo wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanahudhuria Kongamano hilo, ambapo mada mbalimbali zitawasilishwa kwa wajumbe na kujadiliwa katika kongamano hilo na kutolewa mapendekezo ya hatua zitakazochukuliwa , kutoka kulia ni Waziri Mkuu wa zamani Joseph Sinde Warioba, Katibu Mkuu wa chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad ,Katibu mkuu wa Zamani wa AU amabyo zamani ilijulikana kama OAU Salim A. Salim na Mwenyekiti wa Chama hicho Prf. Ibrahim Lipumba.


Msomaji
Dar es salaam

No comments: