Friday, December 4, 2009

maadhimisho wa siku ya walemavu nchini tanzania kwenye viwaja vya Mnazi Mmoja yalivyofana!!

Mkuu wa wilaya ya Ilala Evance Balama akimuangalia Abdala Nyangala ambaye ni mlemavu wa macho kutoka Mbagala Kibondemaji jinsi anavyochomeka uzi wa sherehani kwenye cherehani yake ambayo anaitumia kushona nguo za aina mbalimbali za jinsia ya kike na kiume. Mkuu wa wilaya huyo alikuwa mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya walemavu Duniani yaliyofanyika leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI (TACAIDS) Fatma Mrisho akiangalia batiki zilizotengenezwa na wanawake wajasiliamali wenye ulemavu wa aina zote wakati wa maadhimisho ya siku ya walemavu Duniani yaliyofanyika leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa kikundi cha sanaa cha walemavu wa aina zote cha Upendo kilichopo mkoani Dar es Salaam wakitoa burudani wakati wa maadhimisho ya siku ya walemavu Duniani yaliyofanyika leo katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Msomaji
Dar es salaam

No comments: