Thursday, December 3, 2009

Kigoma Nao Pia Wagoma !!

Wasafiri wakiwa katika stesheni ya Kigoma wakisubuli usafiri wafanyakazi wamegoma hadi wapewe malipo yao na kampuni mpya ya kuendesha shirika hilo.Treni ya abiria ya kwenda Mwanza, Kigoma na Mpanda ikiwa imesimama katika stesheni ya Salanda mkoani Singida ili abiria wajipatie chakula juzi. Treni hiyo iliingia mkoani Kigoma jana baada ya madereva wake kuwa na mgomo katika vituo vya njiani mara kwa mara.
Jamani wafanyakazi wa Reli ya kati wanananyanyasika sana kwa kuchelewaeshewa malipo yao ya mishahara. hadi wamefikia uamuzi wa kugoma kushinikiza walipwe stahili zao
Baadhi ya abiria waliokuwa wakisafiri kuelekea Kigoma na Mwanza wakiwa wamezonga stesheni ya Manyoni baada ya dereva wa treni kugoma wakati walipofika eneo hilo wakidai kuwa hadi shirika hilo liwalipe mshahara wa mwezi wa November.
Huku hakuna magari ya kutoa upepo kama vile mgoma wa Dar.
vurugu kwenda mbele.
Abiria wakiwa ndani ya mabehewa wakisubiri hatima yao ya safari yao.

Msomaji
Kigoma

No comments: