Friday, December 4, 2009

Balozi wa Marekani Akutana na Rais Karume

Balozi Mpya wa Marekani Nchini Tanzania Mhe Alfonso Lenhardt jana alimtembelea ikulu Rais wa Zanzibar Mh Amani Abeid Karume na kumweleza jinsi serikali ya nchi ya Marekani imeridhishwa na utaalamu unaotumika katika uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura linaloendelea visiwani Zanzibar. Balozi huyo pia alisifu jinsi zoezi hilo linavyoendelea kwa amani na utulivu katika maeneo mbalimbali katika vituo kadhaa alivyovitembelea alipowasili visiwani Unguja kabla ya kwenda ikulu kuonana na rais.

Msomaji
Zanzibar

No comments: