Friday, December 4, 2009

Balozi wa Rwanda aishukuru Tanzania

Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Bi. Fatuma Ndangiza akitoa tamko rasmi la Rwanda kujiunga na Jumuiya ya Madola na pia kushukuru mchango wa Tanzania kusaidia kufanikisha zoezi hilo leo jijini Dar es salaam. Rwanda sasa ni mwanachama wa 54 wa Jumuiya ya Madola kufuatia kukubaliwa na wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola katika mkutano uliofanyika Trinidad na Tobago.

Msomaji
Dar es salaam

No comments: