Sunday, June 14, 2009

WATAALAM KUTOKA JAPAN WALIVYOAGWA NA KAIMU KATIBU MKUU MENEJIMENTI YA UTUMISHI

Mmoja wa wataalamu wa kujitolea katika fani mbalimbali waliokuja nchini kutoka Japan Yuka Nakayama akifurahia Zawadi yake aliyokabidhiwa na Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma Mathias Kabunduguru baada ya kumaliza muda wa miaka miwili ya kujitolea nchini Tanzania.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma Mathias Kabunduguru akiongea na wataalam wa fani mbalimbali kutoka nchini Japan waliokuja nchini kujitolea.Wataalamu hao walikuwa wakijitolea katika nyanja mbalimbali za sayansi ikiwemo ualimu wa shule za sekondari,sekta ya afya, masuala ya jamii na fani za mawasiliano na wanatarajia kuondoka nchini tarehe 17 mwezi huu.

Msomaji
Dar es salaam

No comments: