Saturday, June 27, 2009

KAIMU SHEIKH MKUU WA TANZANIA AFARIKI DUNIA.

Aliyekuwa kaimu sheikh mkuu wa Bakwata mzee Suleiman Gorogosi amefariki dunia kwa ajali ya gari iliyotokea leo mchana (EastAfrican Time) akiwa njiani kwenda Lindi. Sheikh Gorogosi alikuwa akitokea Mtwara ambapo alikuwa amewasili muda mchache kwa ndege toka Dar es salaam, hata hivyo taarifa hiyo haikusema mzee Gorogosi alikuwa katika safari binafsi au ni ya kikazi na kama gari hilo lilikuwa ni binafsi au ni la jumuia (private car or public trasport). tutawaletea taarifa zaidi pindi zitakapo tufikia.

No comments: