Msomaji
Dar es salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete(Watano kulia) Rais Wa Zanzibar Amani Abeid Karume (Wasita kulia),pamoja viongozi wengine wa kitaifa wakiomba dua katika kaburi la muasisi wa mapinduzi ya Zanzibar Hayati Mzee Abeid Amani Karume huko katika ofisi kuu ya CCm Kisiwandui Zanzibar leo asubuhi.wengine katika picha kutoka kushoto Naibu Waziri kiongozi wa SMZ Ali Juma Shamuhuna,Naibu Katibu mkuu CCM Zanzibar Salehe Ramadhani Feruzi,Waziri kiongozi wa SMZ Shamsi Vuai Nahodha, na makamu wa Rais Dr.Ali Mohamed Shein.
Maghorofa mpya yaliyopo mtaa wa Michenzani Zanzibar yaliyoanza kujengwa kwaajili ya makazi bora ya Wananchi wa Zanzibar na hayati Mzee Abeid Amani Karume na kukamilishwa na Rais wa sasa Amani Abeid Karume.Makazi hayo tayari yamenza kugawanywa kwa wananchi waliokusudiwa kwa utaratibu maalumu 
Rais Jakaya mrisho Kikwete, Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar(kulia) na Mwenyekiti wa jumuiya ya umojawa Vijana wa CCM Bwana Yusuf Masauni wakati wa mapokezi ya maandamano ya umoja wa vijana wa CCM mjini Zanzibar jana jioni.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mwenyekiti wa Jumuiya ya umoja wa Vijana CCM Yusuf Masauni(wapili kushoto), Makamu mwenyekiti wa jumuiya hiyo Bwana Beno Malisa(kushoto), na katibu mkuu wa jumuiya ya umoja wa Vijana CCM Bwana Martin Shigela wakiyapokea maandamano ya vijana wa CCM katika viwanja vya CCM Maisara Zanzibar jana jioni.Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye aliyekuwa mgeni Rasmi katika maandamano hayo aliwahutubia vijana hao.
Baadhi ya vijana wananchama wa UVCCM wakishangilia hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyoitoa wakati wa kilele cha maandamano yaliyoandaliwa na jumuiya hiyo mjini Zanzibar kumuenzi muasisi wa mapinduzi ya zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika mazungumzo na Balozi wa China nchini Tanzania Liu Xinsheng mara baada ya kuwasili Ikulu leo jijini Dar es salaam kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali vikiweo vifaa vya usafiri, vifaa vya nyumbani na michezo vyenye thamani ya shilingi milioni 51.
Rais Jakaya Kikwete akiagalia msaada wa baiskeli zilizotolewa na nchi ya China ikiwa ni sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 51 vilivyotolewa na nchi hiyo leo Ikulu jijini Dar es salaam.Kulia kwake ni Balozi wa China Liu Xinsheng aliyekabidhi msaada huo.
Rais Jakaya Kikwete akikagua pikipiki ikiwa ni sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na nchi ya China kupitia kwa Balozi wa nchi hiyo Liu Xinsheng (kulia) kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo nchini. Makabidhiano hayo ya vitu mbalimbali vikiweo vifaa vya usafiri, vifaa vya nyumbani na michezo vyenye thamani ya shilingi milioni 51 yamefanyika leo Ikulu jijini Dar es salaam
Mgeni Rasmi na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ridhiwani Kikwete akimsimika Kamada wa Vijana CCM kata ya Kijitonyama kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika shule ya msingi Kijitonyama leo jioni makamanda wengine kutoka matawi pia wamesimikwa katika mkutano huo. 
Ridhiwani Kikwete akifurahia kitu na Mnazi mkubwa wa Simba na Mkereketwa wa Chama Cha Mapinduzi Bw. Kipukuswa mara baada ya kumaliza kazi ya kusimika makamanda wa vijana CCM kata ya Kijitonyama wanaofuatia ni Tony Ngombale Mwiru aliyesimikwa kuwa Kamanda wa Vijana Kata ya Kijitonyama na mwisho ni Rehure Nyaulawa aliyesimikwa kuwa kamanda wa tawi la Bwawani.
Mjumbea wa kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Diwani wa kata ya Kijitonyama Omary Kimbau na Mbunge wa Kinondoni Mh Iddi Azan mara baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara kwa ajili ya kusimika makamanda wa vijana kata ya Kijitonyama uliofanyika leo katika shule ya mdsingi Kijitonyama.
Mjumbe wa kamati ya Utekekelezaji Umoja wa Vijana CCM Taifa Ridhiwani Kikwete akifungua Tawi la CCM shule ya Kijitonyama katikata nikamanda wa vijana Kata ya Kijitonyama Tony Ngombale Mwiru na kushoto ni Ismail Mwenda katibu Mwenezi CCM tawi la Bwawani.
Wanachama mbalimbali wakifuatilia kila kilichojiri kwenye mkutano huo.
Wanachama mbalimbali wakifuatilia kila kilichojiri kwenye mkutano huo.