Thursday, March 11, 2010

CCM Singida Mjini waaswa kuepuka makundi

KATIBU wa Siasa na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Singida Mjini, Hassan Mazala amewaasa viongozi waandamizi wa Jimbo hilo kuepuka makundi na baadala yake waendeleze mshikamano ilikuendeleza mshikamano na kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi ujao.Akizungumza katika maojiano maalum juu ya hali ya kisiasa jimboni humo, jana jijini Dar es Salaam , alisema kuwa mpaka sasa Viongozi wameweza kutekeleza ilani ya Chama kwa asilimia kubwa na kuendeleza matumaini kwa wananchi, viongozi hao ni Rais, Mbunge na Madiwani katika Halimashauri hiyo ya Manispaa ya Singida.“Viongozi wote waliochaguliwa mwaka 2005 kupitia CCM, wameweza kutekeleza Ilani kwa asilimia kubwa, zikiwemo ahada zao binafsi. hivyo nawaomba Viongozi na wana CCM tuendeleze mshikamano tulio kuwa nao” alisema Mazala.Mazala aliendelea kusema kuwa, kwa kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu, vuiongozi wa wa juu wa Chama ambao ndiyo wanaokuwa na dhamana ya kupendekleza viongozi kuingia katika michakato mbalimbali, aliwaasa kuachana na makundi pamoja na chuki ambapo kama wataepuka hali hiyo Chama kitaendelea kuimalika.“Unaweza kumshagua kiongozi kwa kutumia ulaghai, lakini je anaweza kutekeleza ilani ya Chama kwa vitendo?, hivyo kama viongozi wanajukumu la kuangalia hilo kwa undani na wala wasiangalie wapi kuna maslai binafsi” alimalizia Mazala.

Msomaji
Singida

No comments: