Tuesday, March 16, 2010

Rais Kikwete apokea jezi ua Real Madrid, akabidhiwa pich yake iliyochorwa, na kumpokea waziri mkuu wa Finland Mhe Matti Vanhanen

Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mstahiki Adam Kimbisa akimkabidhi Rais Jakaya Mrisho Kikwete zawadi ya jezi namba tisa ya Timu ya Real Madrid ya Hispania inayovaliwa na nyota wa timu hiyo Ronaldo ikulu jijini Dar es Salaam leo kwa kutambua mchango wa Rais Kikwete katika kukuza mchezo wa soka nchini
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha ikulu jijini Dar es Salaam Waziri Mkuu wa Finland Matti Vanhanen leo asubuhi baadaye viongozi hao walifanya mazungumzo
Msanii Paul Ndembo ambaye amejikita katika uchoraji wa sura za watu mbalimbali hususan viongozi akimkabidhi Rais Jakaya Kikwete picha aliyoichora.Msanii huyo alimkabidhi Rais Picha hiyo wakati wa hafla fupi iliyofanyika ikulu jijinji Dar es Salaam leo asubuhi. Msanii Paul Ndembo akimuonesha Rais Kikwete moja ya picha alizochora za nyakati mbalimbali za Uongozi wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Picha hiyo imewekwa katika ukuta sehemu ya mapokezi ikulu jijini Dar es Salaam.Msanii Paul Ndembo ni Mhitimu katika kitivo cha Sanaa cha Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda Mwaka 1970 na ni mchoraji mahiri wa stempu za barua Tanzania
Msomaji
Dar es salaam

No comments: