Sunday, March 28, 2010

Ufunguzi rasmi wa mkutano wa 122 wa umoja wa Mabunge Duniani, Bangkok

Spika wa Bunge, Mhe. Samuel Sitta akichangia katika mjadala kuhusu maswala ya kisiasa na kiuchumi Duniani wakati wa Mkutano wa 122 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) unaofanyika mjini Bangkok, Thailand, wikiendi hii.
Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 122 wa IPU katika picha ya pamoja mara baada ya kufunguliwa rasmi jana.

Spika wa Bunge, Mhe. Samuel Sitta, akifuatilia kwa makini ufunguzi rasmi wa mkutano wa 122 wa umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ulioanza rasmi jana mjini Bangkok, Thailand kwa kufunguliwa na Mtoto wa Mfalme wa nchi hiyo, Princess Maha Chakri Sirindhorn . Walioketi kusho ni balozi wa Tanzania nchini Malaysia anayesimamia pia Thailand, Mhe. Cisco Mtiro, Mhe, Dkt Christine Ishengoma, Mhe. Idris Mtulia na Mhe. Suzan Lyimo.
Binti Mfalme wa Thailand, Malkia Maha Chakri Sirindhorn, akifungua rasmi mkutano wa 122 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) katika ukumbi wa Centara Bangkok Convention Centre. Mkutano wa huo umeanza rasmi wikiendi hii kwa kushirikisha wajumbe toka zaidi ya Mabunge ya nchi 150 Duniani.
Msomaji
Thailand

No comments: