Saturday, March 27, 2010

Rais Kikwete alivyozindua kitabu cha historia ya maisha ya utumishi wa umma ya Sir George Kahama ikulu jijini Dar es salaam

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe ulizingushwa kwenye kitabu kinachohusu historia ya maisha ya utumishi serikalini ya Mwanasiasa mkongwe Sir.George Kahama wakati wa hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto waoshuhudia uzinduzi huo ni Rais Mstaafu awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, Mwanasiasa mkongwe Sir.George Kahama(wapili kushoto), Rais Mstaafu awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi(wanne kushoto) na watano kushoto ni Mwandishi wa kitabu hicho ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Royalty Bwana Joseph kahama.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka mezani tayari kwa mauzo kitabu kinachohusu maisha ya Mwanasiasa Mkongwe Sir.George Kahama muda mfupi baada ya kukizindua katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni.kutoka kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya tatu Benjamin Mkapa, Mwanasiasa mkongwe Sir George Kahama(wapili kushoto) na wanne kushoto ni Joseph Kahama ambaye ni mwandishi wa kitabu hicho. Joseph ni Mtoto wa Mzee Kahama.
Joseph Kahama ambaye ni Mwandishi wa kitabu kinachohusu historia ya Maisha ya Utumishi Serikalini ya Mwanasiasa Mkongwe Sir.George Kahama akimkabidhi Mama Maria Nyerere nakala ya kitabu hicho katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuzindua kitabu hicho.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Joseph Kahama(Wanne kushoto) ambaye ni Mwandishi wa kitabu kinachohusu maisha ya mwanasiasa mkongwe Sir.George Kahama wakati wa hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika jijini Dar es Salaam leo jioni.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamim Mkapa, Sir Geroge Kahama(wapili kushoto) na kulia ni Rais Mstaafyu awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi
Msomaji
Dar es salaam

No comments: