Thursday, March 11, 2010

Rais Jakaya Kikwete ziarani Kitunda, Sikonge Mkoani Tabora

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipampu maji kutoka katika kisima kilichonjengwa nawananchi chini mradi unaoratibiwa na shirika la maendelo la umoja wa Mataifa UNDP, katika Kijiji cha Mbola, Wilaynai Uyui, mkoa wa Tabora jana.Anayeangali ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mwakilishi MkaZI wa UNDP Bwana Aberic Kacou.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuzindua ujenzi wa ukarabati wa zahanati ya Kitunda,wilayani Sikonge jana jioni.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua shamba la mahindi lililolimwa kwa ubora na mkulima Bwana Abdallah Sebitango Balakekenwa katikA KIJIJI CHA Mbola KAta ya Ilolangulu, Wilayani Uyui, mkoa wa Tabora.Mkulima huyo mwenye kumiliki shamba la ekari 25 ana wake wawili na Rais Kikwete ameahidi kumnunulia ng’ombe wa kulimia ahadi hiyo ilitimizwa hapo hapo
Kikongwe aliyejitambulisha kwa jina la Bi.Zubeti Kungi akisalimiana na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete pamoja na Rais Kikwete muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kuhutubia mkutano wa hadhara, katika eneo la Kitunda, Wilayani Sikonge.Bi Kungi alisema kuwa amezaliwa mwaka 1936 na kuwa alifurahi sana kumuona na kusalimiana na Rais Kikwete pamoja na mkewe.
Msomaji
Tabora

No comments: