Wednesday, March 10, 2010

TONY NGOMBALE MWIRU ASIMIKWA KUWA KAMANDA WA VIJANA CCM KATA YA KIJITONYAMA

Mgeni Rasmi na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ridhiwani Kikwete akimsimika Kamada wa Vijana CCM kata ya Kijitonyama kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika shule ya msingi Kijitonyama leo jioni makamanda wengine kutoka matawi pia wamesimikwa katika mkutano huo.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ridhiwani Kikwete hapa akimvisha ukamada wa Tawil la Bwawani Rehure Nyaulawa.
Ridhiwani Kikwete akifurahia kitu na Mnazi mkubwa wa Simba na Mkereketwa wa Chama Cha Mapinduzi Bw. Kipukuswa mara baada ya kumaliza kazi ya kusimika makamanda wa vijana CCM kata ya Kijitonyama wanaofuatia ni Tony Ngombale Mwiru aliyesimikwa kuwa Kamanda wa Vijana Kata ya Kijitonyama na mwisho ni Rehure Nyaulawa aliyesimikwa kuwa kamanda wa tawi la Bwawani.
Mjumbea wa kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Diwani wa kata ya Kijitonyama Omary Kimbau na Mbunge wa Kinondoni Mh Iddi Azan mara baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara kwa ajili ya kusimika makamanda wa vijana kata ya Kijitonyama uliofanyika leo katika shule ya mdsingi Kijitonyama.
Mjumbe wa kamati ya Utekekelezaji Umoja wa Vijana CCM Taifa Ridhiwani Kikwete akifungua Tawi la CCM shule ya Kijitonyama katikata nikamanda wa vijana Kata ya Kijitonyama Tony Ngombale Mwiru na kushoto ni Ismail Mwenda katibu Mwenezi CCM tawi la Bwawani.
Wanachama mbalimbali wakifuatilia kila kilichojiri kwenye mkutano huo.
Wanachama mbalimbali wakifuatilia kila kilichojiri kwenye mkutano huo.
Wakereketwa mbalimbali wa chgama cha mapinduzi wakiserebuka na muziki wa taarab wakati makamnda wa vijana wa kata ya Kijitonyama waliposimikwa rasmi jioni leo katika mkutano uliofanyika katika shule ya msingi Kijitonyama.
Msimaji
Dar es salaam

No comments: