Tuesday, April 7, 2009

Key Speakers of the plenary session

Jakaya Kikwete, President, United Republic of Tanzania
President Jakaya Mrisho Kikwete was inaugurated on December 21st, 2005 as the Fourth President of the United Republic of Tanzania. In his more than 30 years of public service, President Kikwete led key portfolios in successive governments including Minister for Finance and Minister for Water, Energy and Mineral Resources. He was elected Member of Parliament for 15 consecutive years, from 1990 to 2005. In January 31, 2008, President Kikwete was elected by Heads of States and Government of Africa to be the Chairman of the African Union (AU) for 2008.

Asha-Rose Migiro, is the Deputy Secretary-General of the United Nations. Before that, she served as Tanzania’s Minister of Foreign Affairs and International Cooperation. Dr. Migiro also pursued a career in academia, serving as a Senior Lecturer at the Faculty of Law at the University of Dar-es-Salaam. She has a Master of Laws from the University of Dar-es-Salaam and a Doctorate in law from the University of Konstanz in Germany. Abdoulaye Diop, Finance Minister, Senegal. Mr. Abdoulaye Diop has served in the government of Senegal since May 2000 and as Minister of Economy and Finance since May 2001. Prior to his appointment in the government, Mr. Diop served in the Public Accounting Office and in the Treasury. He has also represented Senegal in many international financial institutions, including the World Bank, the IMF, and the African Development Bank Akere Muna, AU Civil Society Advisory Panel. Mr. Akere Muna is the Presiding Officer of the Economic, Social and Cultural Council of the African Union. A lawyer by training, he has previously held the post of President of Transparency International Cameroon, and currently serves as a member of the Board of Directors of Transparency International. Previously, he was president of the Pan-African Lawyers' Union. Benno Ndulu, Governor, Bank of Tanzania. Prior to that, he served as an Advisor to the Vice President, African Region of the World Bank and as the Manager of Partnerships Group. He is best known for his involvement in setting up one of the most effective research and training networks in Africa.Chukwuma C. Soludo, Central Bank Governor, Nigeria. He previously served as the Economic Adviser to President Obasanjo and was the Founding Director of the African Institute for Applied Economics, Enugu, Nigeria. Before joining government he was Professor of Economics at the University of Nigeria, Nsukka. Professor Soludo’s research spans a wide set of topics in African development, with a focus on macroeconomic management, monetary/financial policies and international trade. Professor Soludo has been appointed Member of the Chief Economist Advisory Council of the World Bank and recently has been also appointed by the President of the UN General Assembly as a member of the 10-man Commission of Experts on the Reform of the International Monetary and Financial System.Donald Kaberuka is the 7th President of the African Development Bank. He served as Rwanda’s Finance and Economic Planning Minister from 1997 to 2005, and played a major role in leading the economic team responsible for the successful reconstruction of the country in the aftermath of the 1994 genocide. Since his election at the Bank, Dr. Kaberuka has carried out major reforms to refocus the African Development Bank’s agenda on regional economic integration, private sector, infrastructure, governance, and a special initiative for post conflict countries and fragile states. Dominique Strauss-Kahn, Managing Director, International Monetary Fund Dominique Strauss-Kahn assumed office as the tenth Managing Director of the International Monetary Fund on November 1, 2007. Upon being selected by the IMF's Board of Executive Directors, Mr. Strauss-Kahn indicated that he will press ahead with reform of the 185-member country institution that helps oversee the global economy.

Festus Mogae, Former President of Botswana. Mr. Festus G. Mogae was president of Botswana from 31st March 1998 to 31st March 2008. He served in Washington, DC as Alternate and the Executive Director, International Monetary Fund for Anglophone Africa from 1976 to 1980. He was Governor of the Bank of Botswana from 1980 to 1981. From 1982 to 1989 he was Permanent Secretary to the President, Secretary to the Cabinet and Supervisor of Elections. Mr. Mogae joined politics in 1989 and was appointed Minister of Finance and Development Planning and became Vice President in 1992. Goodall Gondwe, Finance Minister, Malawi . Mr. Goodall Edward Gondwe has served in the Government of Malawi since 2002 and as Minister of Finance since 2004. Previously he was director of Africa Department at the International Monetary Fund, and Vice President of the African Development BankJeffrey Sachs, Columbia University. Jeffrey D. Sachs is the Director of The Earth Institute and Professor of Sustainable Development and Health Policy and Management at Columbia University. He is also Special Advisor to United Nations Secretary-General Ban Ki-moon on the Millennium Development Goals, the internationally agreed goals to reduce extreme poverty, disease, and hunger by the year 2015. From 2002 to 2006, he was Director of the UN Millennium Project and Special Advisor to United Nations Secretary-General Kofi Annan. Sachs is also President and Co-Founder of Millennium Promise Alliance, a nonprofit organization aimed at ending extreme global poverty. Kofi Annan, President of Global Humanitarian Forum, UN Secretary-General (1997-2007) Kofi A. Annan of Ghana, the seventh Secretary-General of the United Nations, served from 1997 to 2006 and was the first to emerge from the ranks of United Nations staff. Mr. Annan was awarded the 2001 Nobel Prize for Peace jointly with the United Nations. Linah Mohohlo, Governor Central Bank of Botswana
Ms. Linah Mohohlo has been the Governor of the Bank of Botswana since 1999 following a 23-year career with the Bank and, in her capacity as Governor of the IMF for Botswana, she has been a member of the International Monetary and Financial Committee (IMFC) representing the Africa Group 1 Constituency.
Manuel Chang, Finance Minister, Mozambique. Mr. Manuel Chang was appointed Minister of Finance of Mozambique in February 2005. Previous posts include: Vice Minister of Planning and Finance; National Director of the Treasury; and National Director of Budget. He has served as the Chairman of the General Assembly of the Commercial Bank of Mozambique and the Chairman of the Auditor Council of the Bank of Mozambique.
Mo Ibrahim, Founder of Mo Ibrahim Foundation Dr. Mo Ibrahim is a global expert in mobile communications and founding chairman of Satya Capital, an investment company focused on opportunities in Africa. Sudanese by birth, Dr Ibrahim is the founder and former chairman of Celtel International, one of Africa’s most successful companies. In 2006 he set up the Mo Ibrahim Foundation to support great African leadership. The Foundation focuses on two major new initiatives to stimulate debate around, and improve the quality of, governance in Africa.
Michael Joseph is the CEO of Safaricom Limited and has been in this position since July 2000 when the company was re-launched as a joint-venture with Telkom Kenya. Since the re-launch of Safaricom in October 2000 he has guided the company from a subscriber base of fewer than 20,000 to 12,935,861 as of 11th Jan 2009, including the launch of many award winning innovative products and services over the past 8 years. Today Safaricom is one of the leading companies in East Africa and is the most profitable company in the region.Naushad.N Merali, Chairman & CEO of the Sameer Group is one of Kenya’s leading industrialists. The Sameer Group is a conglomerate of companies with major investments and successful operating organizations in all-key sectors of the economy. The Group has been at the very heart of Kenya's industrial and commercial development for over thirty years and continues to expand its business throughout the East African region.Ngozi Okonjo-Iweala is presently a Managing Director of the World Bank. From September 2006 to November 2007, she was Distinguished Visiting Fellow at Brookings Institution. From June to August 2006, she was Minister of Foreign Affairs of Nigeria, overseeing Nigeria’s External Relations and from July 2003 to June 2006 she served as Minister of Finance and Economy of Nigeria and Head of Nigeria's much acclaimed Presidential Economic team responsible for implementing a comprehensive home grown economic reform program. Previously, she pursued a 21-year career as a development economist at the World Bank, where she held the post of Vice President and Corporate Secretary.
Nemat Shafik, Permanent Secretary, Department for International Development, UK Nemat (Minouche) Shafik was appointed in March 2008 as Permanent Secretary of the Department for International Development which is responsible for leading the British government’s fight against world poverty. She is responsible for development programmes and policy work on the United Nations system, the international financial institutions, Europe, country assistance, civil society, trade, conflict prevention, and climate change. Prior to this, she was Director General, Country Programmes in DFID where she was responsible for all of the UK’s aid to countries delivered through 1800 staff in 67 offices around the world.Paul Collier is Professor of Economics, Oxford University Economics Department and Director of the Center for the Study of African Economies. His academic work focuses on the causes and consequences of civil war; the effects of aid; and the problems of democracy in low-income and natural-resource-rich societies. Mr. Collier's policy work has included a post as senior adviser to Blair’s Commission on Africa, where his work covers a wide range of macroeconomic, microeconomic and political economy topics concerned with Africa. Peter Eigen, Chairman, EITI Prof. Dr. Peter Eigen is a lawyer by training. He has worked in economic development for 25 years, mainly as a World Bank manager of programs in Africa and Latin America. In 1993 Eigen founded Transparency International (TI), a non-governmental organization promoting transparency and accountability in international development. In 2005, Eigen chaired the International Advisory Group of the Extractive Industries Transparency Initiative (EITI) and became Chair of EITI in 2006 Salaheddine Mezouar, Finance Minister, Morocco Mr. Salaheddine Mezouar was named Moroccan Minister of Economy and Finance in 2007. Previously he held the post of Minister of Industry and Trade and is the former president of the Moroccan Association of Textile and Clothing Manufacturers. He has held positions in both the public and private sector in Morocco. Trevor Manuel, Finance Minister, South Africa Mr. Trevor Manuel was elected a Member of Parliament in South Africa's first democratic elections, and in May 1994, he was appointed Minister of Trade and Industry. He was appointed Minister of Finance in April 1996. In his capacity as Minister of Finance, Mr. Manuel serves as a Governor on the Board of the World Bank Group, the African Development Bank Group and the Development Bank of Southern Africa, and is also Chairman of the World Bank Development Committee.
Valentine Rugwabiza is the Deputy Director-General of the World Trade Organization. In this role, which she took up in October 2005, her responsibility covers development issues and policies generally; trade policy review; trade facilitation, and training and technical cooperation. She is also responsible for the WTO work program on Aid for Trade. Prior to her current post, Mrs. Sendanyoye Rugwabiza served for three years simultaneously as Rwanda's Permanent Representative to the UN in Geneva, Head of Delegation to the WTO and Ambassador Extraordinary and Plenipotentiary to Switzerland.

Venue: Dar es Salaam, Tanzania

Date: March 10–11, 2009.

Hosts: United Republic of Tanzania and International Monetary Fund

Ndejembi Michael.

Monday, April 6, 2009

UBALOZI WA RWANDA KUCHANGISHA FEDHA KUSAIDIA YATIMA WA MAUAJI YA KIMBARI YA MWAKA 1994

Balozi wa Rwanda Nchini Zeno Mutimura akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari maelezo leo juu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini humo mwaka 1994 miaka 15 iliyopita yanayotarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Karimjee jijini
Nakaaya Sumari akielezea wandishi wa habari juu ya wimbo wake wa I am in Africa alioutunga maalum kwa ajili ya kampeni ya kusaidia yatima waliotokana na mauaji ya kimbari mwaka 1994 nchini Rwanda ubalozi wa Rwanda na umoja wa mataifa wataadhimisha kukumbuka mauaji hayo kesho kwenye ukumbi wa Karimjee jijini.

Kutoka kulia ni wanamuziki Enika Bukuku, Chid Benz, Nakaaya Sumari na Sauda Simba Nakaaya ametunga wimbo unaoitwa I am in Africa unaowaonya waafrika kutothubutu kufanya mambo ambayo yanaweza kupelekea mauaji ya Kimbari kama yaliyotokea nchini Rwanda miaka 15 iliyopita lakini pia kuhamasisha waafrika wakiwemo Tanzania kuchangia japo dola moja tu kwa ajili ya kusaidia yatima waliopoteza wazazi kutokana na mauaji


Balozi wa Rwanda Nchini Zeno Mutimura alizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya habari maelezo leo juu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini humo mwaka 1994 miaka 15 iliyopita yanayotarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam
Katika maadhimisho hayo pia kutakuwa na wimbo maalum uliotungwa na mwanamuziki Nakaaya Sumari unaoitwa I am in Africa kuachana na mambo ambayo yanaweza kuchochea kwa mauaji kama yaliyotokea Rwanda laakini pia unaozungumzia kampeni ya kuwasaidia yatima walioko nchini Rwanda waliopoteza wazazi kutokana na mauaji hayo watu mbalimbali na mashirika wameombwa kuchangia kuazia dola moja na kuendelea.
Balozi Mutimura amezitaja akaunti zitakazotumika kukusanya michango hiyo kuwa ni National Bank of Commerce Emassy of Rwanda Acc No. USD:012105025668 na Acc no: Tsh: 012103016937 kampeni hii itaendeshwa kwa muda wa siku 100 ili kukusanya michango hii katika picha kushoto ni Usia Nkhoma afisa habari wa umoja wa mataifa.
Msomaji
Dar es salaam

Kenyan Vice-President Says Arusha, Tanzania Will Serve As EAC Headquarters

Arusha will continue to serve as the headquarters of the East African Community because that is provided in the treaty to establish the community.

Kenyan Vice President Stephen Kalonzo Musyoka last week said ideological and economic differences among the EAC member countries should be ironed out and not allowed to undermine the economic and political integration process.

He made the remarks when he opened the Third East African Health and Scientific Conference attended by ministers and other senior officials from the five partner states-Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda and Burundi.

He warned that detractors of the Community were using such differences to plant elements of mistrust. He cited recent reports of some member states challenging the suitability of Arusha as EAC seat.

"We struggled hard to regain our confidence and revive the Community in Arusha", he told hundreds of delegates at the Kenyatta International Conference Centre.

He added that dictators and maverick leaders like Idi Amin, the former military ruler of Uganda in EA were now rare species in the region.

The late dictator Amin sent his forces to invade and occupy parts of Kagera region in 1978 few years after he had threatened to annex nearly one third of Kenya.

Mr. Musyoka also called for the promotion of Kiswahili as one of the languages of the African Union as once adopted in one of the AU summits.

He said Kiswahili, as medium of communication, could unite the people of EA and in that vein speed up the integration process.

He lauded Tanzania and some radio stations based abroad for spearheading the promotion of Kiswahili, adding that EAC has already established a special body under its secretariat on Kiswahili research.

Tanzanian delegation to the three-day conference comprised four ministers including Dr. Batilda Buriani, the minister of states in the Vice President's Office (Environment).
Relevant Links

Others are the deputy ministers; Dr. Maua Daftari, Communications, Science and Technology; Dr. Asha Kigoda, ministry of Health and Social Welfare and Mohamed Abood, the deputy minister for East African Cooperation.

Recently in Mombasa Mr. Musyoka stressed that there was no controversy on Arusha as EAC headquarters because the Treaty that established the regional body clearly stipulated the northern town as its permanent seat.

Msomaji
Arusha

WAZIRI MKUU MH. MIZENGO KAYANZA PETER PINDA ALIPOONGEA NA WANARUKWA!!

Waziri mkuu Mizengo Pinda akiongea na wana- Rukwa waishio Dar es salaam (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali yahusuyo mkoa wa Rukwa leo jijini Dar es salaam
Wabunge Chrisant Mzindakaya na Anna Lupembe wote kutoka mkoa wa Rukwa wakisalimiana wakati wa mkutano wa wana – Rukwa waishio jijini Dar es salaam.Mkutano huo ambao mwenyekiti wake alikuwa waziri mkuu Mizengo Pinda umefanyika leo jijini Dar es salaam katika ukumbi wa JKT Mgulani.
Waziri mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya washiriki waliohudhuria mkutano wa wana – Rukwa uliofanyika leo katika ukumbi wa JKT Mgulani jijini Dar es salaam.
Wakazi wa Rukwa waishio jijini Dar es salaam wakimsikiliza Waziri mkuu Mizengo Pinda (hayupo pichani) wakati wa mkutano wao uliofanyika leo jijini Dar es salaam.

Msomaji
Dar es salaam

PONGEZI KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA.

Uongozi ulio bora na wenye tija, siku zote ni ule wa wale wenye Dola (wananchi) kuwa na maamzi ya namna dola yao wenyewe iendeshwe katika ngazi mbalimbali za kisiasa, kiuchumi na hata kiutamaduni.
Kwa maana halisi ni kwamba misingi imara ya uchumi bora na endelevu itatoka kwa wananchi wenyewe kwa kupitia viongozi wale waliowachagua wenyewe, toka katika hatua za awali na maamuzi yao kueshimika mpaka katika hatua za kitaifa. Hii itamfanya kiongozi huyo kuwajibika ipasavyo kwa wananchi.
Kwa njia hi itapelekea wananchi kueshimiwa na viongozi wao, kwa kuwa wao ndio watakuwa wenye mamlaka ya kupendekeza viongozi wao kupitia matawi yao.
Napenda kutoa pongezi kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Mh. Mrisho Jakaya Kikwete kwa kuwa na mwelekeo mzuri kwenye hatua za kupata viongozi wa kitaifa wa CCM au wagombea wa kitaifa wa CCM. Hii inaonyesha wazi jinsi gani serikali ya CCM ilivyodhamilia kuwapa wananchi wenyewe nguvu ya kuendesha dola yao kwa kuteua na kupendekeza viongozi wao kuanzia hatua ya Matawi na Mashina.
Hivyo basi napenda kuwaomba wananchi wote kuunga mkono hoja hii kwa vitendo yaani;

(1) Kuhakikisha viongozi watakao wapendekeza wasiwe ni wale ambao wanatoa mlungula (rushwa) ili waweze kupendekezwa na kigezo cha kutoa mlungula kiwe ni sababu mojawapo ya kumnyima kabisa uongozi mtu wa namna hiyo kwani uongozi ni kipawa kutoka kwa Mungu, hivyo kipawa huwa hakiuzwi bali kinajinadi kwa sera nzuri na endelevu.

(2) Kwa kuwa hatua hii inakusudia kabisa kuletwa kwenye matawi, hivyo basi kiongozi atakayeteuliwa awe ni mtu mwenye sifa nzuri kwenye familia yake na si kwa sababu anapesa nyingi la hasha, bali ni kwa uwezo wake wa kuweza kuitunza familia yake kwa misingi ya usawa kielimu, kijinsia, kiuchumi na kimaradhi. Hii ni rahisi kwa wananchi walio karibu na mgombea huyo kuyafahamu yote hayo kwa kuwa ni majirani zake.

(3) Kama mgombea huyo anafanya biashara binafsi wananchi wa eneo husika Pendeni kufahamu kuwa hizo biashara zake ni za kihalali kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo;
a. Zimesajiliwa na zina leseni
b. Je analipia kodi ipasavyo
c. Mahusiano yake na wafanyakazi ni mazuri.
Kwa kufanya hivyo itawasaida kupendekeza viongozi waadilifu ambao wataweza kusimamia kodi zetu ipasavyo, miradi mbalimbali pia itaweza kusimamiwa na kukamilika ipasavyo.

(4)Wananchi pia wawe makini kuangalia je kiongozi watakaowachagua wanayo sifa ya kushirikiana vizuri na majirani zake, hasa katika nyanja za kijamii kama misiba, sherehe za harusi, harambee mbalimbali na shughuli za uzalishaji katika jumuia zetu.

Kwa njia hizi chache na nyinginezo nyingi, zikizingatiwa zitaweza kujenga CCM imara yenye viongozi bora na kama ilivyozoeleka kuwa na majina yale yale yaliyowaletea tija wananchi. Tafadhali wananchi tuwe makini kwenye jambo hili, kwani lina manufaa kwa nchi, na hasa ikizingatiwa kuwa viongozi bora watatoka CCM. Hivyo tuunge mkono hoja hizo za Mwenyekiti wa CCM Taifa Mh. J.M Kikwete vitendo, kwa kuchagua viongozi walio bora, ili waweze kushirikiana na waweze kuliletea tija taifa letu.

Napenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa viongozi wa CCM kwa ushirikiano wenu mzuri kwa Mwenyekiti wa taifa wa CCM -

Nasema, kidumu Chama Cha Mapinduzi.

Anthony N. Rugimbana
Houston Tx
USA.

Friday, April 3, 2009

Tanzania gets taste of NCAA tournament through Thabeet

Thabeet Might Be The Best TAKING A DEFENSIVE TONUConn Thabeet prepare for Senior Day UConn Men's Hoops Notebook: Thabeet impresses at the game UConn needs to rebound from Thabeet Miles Cleared For UConn by Thabeet UConn Motivated To Stay On Top by this men wearing blue
DETROIT — The word from Tanzania is that the people have Final Four fever. Now that they know what it means.

"Even the older people are excited," Lawrence Cheyo said over the phone, as secretary general of the Tanzania Basketball Federation. "For the first time, people are following the NCAA. They watch the NBA here, but they are starting to realize what the NCAA is."

All this buzz, of course, surrounds Connecticut's 7-3 Hasheem Thabeet. Back home, about the only thing taller is Mount Kilimanjaro. As Michigan State coach Tom Izzo said Thursday, "My luck, we would run into a team that's got a 12-foot center."
Thabeet's strange road to Ford Field has become the stuff of Big East legend; the former soccer player from Africa who did not start playing basketball until 15, and once pursued opportunity in America by randomly e-mailing college coaches he found on a Google search. This while working odd jobs as a club bouncer and runway model, supporting the family after his father died.
Now he is 22, Big East co-player of the year as a junior and two games from the national championship. In Tanzania, those with access to the broadcasts will be watching at 1 a.m. Sunday, when Connecticut meets Michigan State. Those who don't will check radios, newspapers, computers, word of mouth.

Msomaji
Mike Lopresti, Gannett

Africa: Why Belief in Witchcraft Remains Strong Among Africans

Henry Makori
3 April 2009

During his recent visit to Africa, Pope Benedict XVI spoke in Angola about many Africans "living in fear of spirits, of malign and threatening powers. In their bewilderment they end up even condemning street children and the elderly as alleged sorcerers. Who can go to them to proclaim that Christ has triumphed over death and all those occult powers?"

The pope was expressing his concern about the persistence of the belief in witchcraft among Africans. This belief is certainly widespread throughout the continent. In Kenya, hardly a day passes without news reports of this phenomenon, especially the harassment of suspected witches.

Since mid-2007, children have been kidnapped and murdered in Uganda in what are believed to be bizarre rituals to attain wealth. In Tanzania, the killing of albinos whose body parts are reportedly used to make charms has caused global consternation.

And last month, Amnesty International found out that up to 1,000 suspected witches in The Gambia had been kidnapped from their villages by witchdoctors employed by the government in a nationwide witch-hunting campaign.

Perhaps more astonishing for Christians was the revelation in 2006 by the bishops of southern Africa that "some Catholic priests act as Sangomas and call on the ancestors for healing.

" A Sangoma is a traditional diviner-healer whose many functions include counteracting witches.
But even when witchcraft is not making the headlines, it is still a daily issue in Africa.

The southern African bishops noted that "many African Christians, during difficult moments in their lives, resort to practices of the traditional religion: the intervention of ancestral spirits, the engagement of spirit-mediums, spirit-possession, consulting diviners about lost items and about the future, magical practices and identifying ('smelling out') one's enemies, etc."

Last year, Cardinal Polycarp Pengo of Dar es Salaam, Tanzania, and president of the Symposium of Episcopal Conferences of Africa and Madagascar (SECAM) decried "the phenomenon common in many African societies of Christianity on Sunday morning and the practice of witchcraft and sorcery during the rest of the week."

Why does belief in witchcraft persist? The attitude of mainstream Christianity is that witchcraft is a vestige of African 'backwardness', the evidence of incomplete conversion or relapse to 'paganism'. More pastoral attention would stamp out the menace.

Witchcraft is also dismissed as ignorant superstition or fear of the unknown. The practitioners and their victims believe in powers that simply do not exist. Sometimes belief in the dark arts is attributed to mass poverty and state failure to 'modernize' the outlook especially of people living in the rural areas. It is argued that if people were better educated and had access to adequate healthcare they would understand that illness is caused by germs and not witchcraft.

But these explanations miss the biggest point. They fail to place witchcraft within the persistent African worldview. Belief in witchcraft is part and parcel of the moral universe as understood in African Traditional Religion. Contrary to popular belief, African Religion is still alive and well.

In African religious thought, the universe created by God ought to be harmonious, balanced and good. But mysterious evil powers exist that disrupt this order. Evil originates not merely from the breaking of taboos and other laws, but from spiritual, mystical powers at work in the universe.

The eminent Tanzanian theologian Fr. Laurent Magesa explains that witchcraft is supernatural. The witch is a person possessing or possessed of, or by, supernatural forces which he or she uses knowingly or unknowingly, selectively or indiscriminately, to harm others often for no apparent reason. Magesa writes that "evil, in the African perception, is always incarnated; it does not exist except as it exists in the evil person, that is, in the witch."

So, how can belief in witchcraft be eradicated? This is hardly possible. According to Fr. Magesa, "in African Religion, witchcraft must be understood as part of the mystery of the human person". Witchcraft is therefore central to the understanding of morality and ethics among Africans.

"In the African mentality, everything wrong or bad in society and in the world, and most particularly various afflictions, originates in witchcraft. There is no kind of illness or hardship at all that may not ultimately be attributed to witchcraft".

Belief in witchcraft shall therefore persist as long as African Traditional Religion exerts influence on Africans. As it is, most African Christians subscribe to two faith traditions. Perhaps the church should not dismiss witchcraft as superstitious nonsense but instead develop appropriate pastoral responses

RAIS JAKAYA AKIPOKEA HATI ZA UTAMBULISHO WA BALOZI HATTEM ATTALAH

Rais Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa balozi wa Tunisia nchini Hattem Attalah Ikulu leo katikati ni mkuu wa Itifaki Mh. Itatilo Rais pia alipokea hati za utambusho wa balozi wa Sierra Lione nchini Balozi Gbabey Bangali.

Msomaji,

Dar es salaam

MSHITAKIWA WA 11 KESI YA AKINA ZOMBE AMEFARIKI DUNIA

Marehemu Rashid Lema akichechemea huku akisaidiwa na mtuhumiwa mwenzake (ambaye yuko huru sasa) alipokuwa anatoka mahakamani Februari 3 mwaka huu.

SHAHIDI muhimu katika kesi ya mauji ya wafanyabiashara watatu kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva taxi mmoja DC Rashid Lema amefariki dunia leo alfajiri katika hospitali ya saratani Ocean Road jijini Dar es Salaam. Taarifa zilizopatika katika hospitali hiyo kupitia Mkurugenzi wa Tiba hospitalini hapo Dk. Hamza Maunda alisema Lema alifariki majira ya saa kumi alfajiri ambapo alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa saratani. Habari zilizofikia mwandishi wa habari hii inasemekana kuwa taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwake Osterbay jijini Dar es Salaam.
Msomaji
Dar es salaam

Thursday, April 2, 2009

HOTUBA YA RAISI JK YA MWISHO WA MWEZI MARCH.

Ndugu wananchi,
Kwa mara nyingine tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi ya kuzungumza na taifa katika utaratibu wetu wa kila mwezi. Naomba radhi kuzungumza nanyi leo badala ya jana kwa sababu ya shughuli za ugeni wa Gavana-Jenerali wa Nchi rafiki ya Australia, Mama Quentin Bryce aliyetutembelea kuanzia tarehe 30 Machi na kuondoka leo asubuhi. Leo napenda kuzungumzia mambo matatu.

Jambo la kwanza ni mwenendo wa mvua na hali ya chakula nchini. Jambo la pili ni hali ya upatikanaji na uzalishaji umeme nchini. Na, la tatu ni mkutano wa Kundi la Nchi Ishirini Tajiri Duniani au maarufu kwa jina la G-20 kwa lugha ya Kiingereza. Mkutano unaoanza kesho mjini London, Uingereza. Mwenendo wa Mvua

Ndugu Wananchi,
Kwa kawaida hii ingekuwa wiki ya pili katika msimu wa mvua za masika kwa maeneo yanayopata mvua hizo. Mvua ambazo hunyesha kwa wingi na kwa saa nyingi mfululizo. Wakati mwingine hunyesha kwa siku mbili au hata tatu mfululizo. Lakini, ninyi na mimi ni mashahidi kuwa mpaka sasa mvua bado hazijaenea maeneo yote na unyeshaji wake siyo kama ule tuliouzoea.
Ingawaje ni mapema mno kuoneakana tuna mashaka, lakini hali ilivyo inatupa kila sababu ya kuwa na wasiwasi kuwa huenda mvua za masika zitanyesha chini ya wastani. Hata wenzetu wa Idara ya Utabiri wa hali ya Hewa wanaonyesha hofu kuwa huenda mvua za masika zisiwe nzuri kama tunavyotarajia.

Ndugu Wananchi;
Bahati mbaya sana Mikoa inayopata mvua za masika hivi sasa hazikupata mvua nzuri wakati wa msimu wa mvua za vuli mwaka wa jana. Kwa sababu hiyo kilimo katika mikoa hiyo kimeathirika, mavuno yamekuwa chini ya wastani na wako baadhi ya wakulima ambao hawakujaaliwa kupata chochote kabisa.

Katika hali hiyo basi, kama katika msimu wa masika hali itakuwa chini ya wastani, ni dhahiri kwamba kutajitokeza tatizo kubwa kwa upande wa upatikanaji wa chakula na mapato ya wakulima kwa jumla.Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali inafuatilia kwa karibu hali hii na tumekuwa tunajiandaa kuchukua hatua zipasazo.

Tathmini tuliyoifanya baada ya kumalizika kwa msimu wa mvua za vuli katika mikoa 9 ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mara, Shinyanga na Kagera zinaonesha kuwa watu wapatao 279,607 katika wilaya 20 watakabiliwa na upungufu wa chakula katika kipindi cha miezi ya Aprili na Mei 2009.

Mipango ya usambazaji wa chakula katika wilaya hizo zenye upungufu inaendelea vizuri. Serikali inaendelea na itaendelea, kukusanya taarifa za hali ya chakula kutoka wilaya zote nchini na kuzifanyia uchambuzi na kutazama namna ya kuboresha hali ya upatikanaji wa chakula. Tutaendelea kutumia akiba yetu ya chakula kuwahudumia wananchi wenzetu watakaokabiliwa na upungufu wa chakula.

Napenda kuwahakikishia Watanzania wote kwamba tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha hakuna mtu atakayekufa kwa njaa. Aidha, napenda kuzihimiza Halmashauri za wilaya zote nchini kuendelea kutuma Wizara ya Kilimo na Chakula taarifa za hali ya mazao na chakula za wilaya zao kila wiki ili kuwezesha Serikali kujua hali ya chakula nchini. Nawataka Wakuu wa Wilaya kulisimamia ipasavyo zoezi hilo.

Na, Wakuu wa Mikoa wahakikishe linafanyika.Wizara ya Kilimo na Chakula itafanya tathmini ya awali ya hali ya mavuno na chakula kuanzia mwezi ujao. Wanategemea kukamilisha ripoti hiyo mwezi Juni, 2009. Hii pia itaiwezesha Serikali kujipanga kukabiliana na hali ya chakula na mavuno itakayojitokeza.
Wito kwa Wananchi

Ndugu Wananchi;
Napenda kuchukua fursa hii kurudia kusisitiza mambo matano yafuatayo:- Kwanza, kwamba kwa wenzetu wa mikoa ya Rukwa, Ruvuma, Iringa, Mtwara, Kigoma na Kagera ambako mvua imekuwa nzuri, tuitumie vizuri fursa hii kuhakikisha kuwa mavuno yamekuwa mazuri.

Pili,
kwamba katika mikoa yenye matatizo ya upungufu wa mvua naomba wananchi watumie mvua zinazonyesha hivi sasa kupanda mbegu zinazokomaa kwa muda mfupi hasa wapande mazao yanayohimili ukame. Kwa ajili hii, tutilie maanani mazao ya viazi, muhogo, mtama na uwele. Hii itatusaidia kupunguza tatizo la uhaba wa chakula nchini iwapo litatokea.

Tatu,
tutumie kwa tahadhari kubwa chakula tulichonacho nchini. Uhaba wa mvua ukiendelea, hali ya upatikanaji wa chakula nchini haitakuwa nzuri mwaka huu. Na ukizingatia kwamba hali ya chakula duniani kwa ujumla pia siyo nzuri ni muhimu wananchi wenzangu tukawa waangalifu katika kutumia chakula tulichonacho. Ni muhimu kufanya hivyo kwani inawezekana kabisa mtu ukawa na fedha za kununulia chakula nje ya nchi, lakini ukakosa chakula cha kununua.

Nne,
kwa kuwa mazao ya nafaka ndiyo yatakayoathirika zaidi na mwenendo wa mvua, napenda kuchukua fursa hii kuwahimiza na kuwahamasisha watanzania wenzangu kwamba sasa tuongeze matumizi ya vyakula visivyo vya nafaka, kama vile, ndizi, muhogo na viazi.

Na,
Tano,
tuongeze bidii na tija kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula ili tujitosheleze kwa chakula na kuuza akiba nje ya nchi. Tuzingatie kanuni za kilimo bora na tutumie pembejeo za kisasa. Aidha, nawaomba tuendelee kuomba dua Mwenyezi Mungu atujalie mvua itakayonusuru mazao mashambani na kutuepusha na tatizo la upungufu wa chakula mwaka huu.
Hali ya Upatikanaji wa Umeme Nchini

Ndugu Wananchi,
Kwa takriban miezi mwili sasa umeme umekuwa gumzo kubwa hapa nchini. Mjadala umekuwa wa namna mbili.
Kwanza umehusu nia ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans pale Ubungo. Na, pili, umehusu mgao wa umeme unaoendelea tangu tarehe 26 Machi, 2009 mpaka sasa hasa hapa Dar es Salaam na wilaya jirani.
Mgao wa Umeme

Ndugu Wananchi,
Kiini cha kuwepo kwa mgao wa umeme ni kuharibika kwa mitambo miwili ya kuzalisha MW 53 za umeme katika kituo cha kuzalisha umeme cha SONGAS. Jumamosi tarehe 28 Machi, 2009 mtambo mmoja wenye uwezo wa kuzalisha MW 20 ulitengemaa hivyo upungufu umebaki MW 33 kutoka kwenye mashine ya pili.

Taarifa niliyopewa leo ni kuwa hitilafu yake ni kubwa hivyo huenda ikachukua mpaka wiki mbili au tatu au zaidi kutengemaa. Maana yake ni kwamba mgao utaendelea kuwepo kwa kipindi hicho. Hivyo, Ndugu zangu, mgao huu hauna uhusiano na ile hadhari aliyoitoa Dkt. Idris Rashid, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alipokuwa akizungumzia suala la Dowans kuwa nchi inaweza kuingia kwenye giza siku za usoni.

Ndugu Wananchi;
Kwa mujibu wa wataalamu wa TANESCO, mfumo wetu wa umeme nchini, kwa sasa, hauna ziada ya umeme unaosubiri kutumika kama akiba. Kutokana na hali hiyo, kunapotokea upungufu wowote wa uzalishaji wa umeme kwa sababu yoyote ile, kama huu uliotokea tarehe 26 Machi, 2009, husababisha kuwepo kwa mgao wa umeme kwa watumiaji.
Umeme wote unaozalishwa hapa nchini hutumika na wala mahitaji halisi hayajatoshelezwa. Kimsingi umeme unaopatikana na kutumika ni chini ya mahitaji (supressed demand). Ni asilimia 14 tu ya Watanzania ndiyo wanaopata na kutumia umeme wakati watu wengi sana wanaohitaji umeme bado hawajapata.

Ndugu Wananchi;
Wakati wote Serikali kwa kushirikiana na TANESCO imekuwa na mipango ya kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini. Kwa upande wa uzalishaji kumekuwepo hata na ratiba ya lini, kituo kipi na cha ukubwa gani kinaratajiwa kuwepo. Utekelezaji wa mipango hiyo ndiyo iliyotufikisha hapa tulipo sasa.
Mwaka 2007, kufuatia matatizo makubwa ya umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji, mpango huo ukaboreshwa na kuongezwa ujenzi wa vituo vya kutumia gesi asilia na makaa ya mawe. Utekelezaji wa mpango wa uzalishaji wa umeme kwa mujibu wa uboreshaji uliofanywa mwaka 2007 uko nyuma ya wakati.

Mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 200 kwa kutumia makaa ya mawe Kiwira umechelewa kwa sababu ya ugumu wa kupata mikopo kutoka kwenye vyombo vya fedha. Kiini cha tatizo ni hofu inayotokana na taarifa hasi kuhusu mradi huo. Mradi wa kuzalisha megawati 300 kutokana na gesi asilimia ya Mnazi Bay unacheleweshwa na matatizo ya sasa ya kudorora kwa uchumi wa dunia ambapo nimeambiwa kwamba wabia muhimu wamejitoa kwa sasa.

Ndugu Wananchi,
Kuchelewa kutekelezwa kwa miradi hiyo ni dalili kuwa baada ya muda si mrefu hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa mbaya hata kama mitambo yote ya sasa itakuwa inafanya kazi kwa ukamilifu. Kwa sasa mahitaji yanaongezeka kwa asilimia 10 – 15 kwa mwaka. Hili ni ongezeko kubwa sana ambalo linahitaji kusiwepo kukwama kokote. Kwa nia ya kutaka kupunguza makali ya tatizo hilo, ndipo uongozi wa TANESCO ukaona waombe kununua mitambo ya Dowans ambayo wakati huo ilikuwa inatangazwa kuuzwa.
Uamuzi huo ukazua mtafaruku mkubwa ambao sina haja ya kuelezea kwa kirefu kwani wengi wetu tunaufahamu vizuri. Baada ya kuona ugumu wa kuendelea na nia hiyo, uongozi wa TANESCO umechukua uamuzi wa kuachana na nia yao hiyo.

Ndugu Wananchi;
Katika taarifa yake ya kutamka uamuzi wa kuachana na nia ya kununua mitambo ya Dowans, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO alielezea hofu yake kwamba uamuzi huo unaweza kusababisha nchi kuwa gizani hapo baadaye.
Taarifa hiyo imeleta hofu kubwa katika jamii. Nataka kuwatoa hofu na kuwahakikishia Watanzania wenzangu wote kuwa Serikali itafanya kila iwezalo kuhakikisha kuwa nchi yetu haifikii hatua hiyo. Tutahakikisha kuwa nchi haiwi gizani na kwamba umeme wa ziada unaotakiwa utapatikana na shughuli za uzalishaji mali na utoaji huduma zitaendelea kama kawaida.

Ndugu Wananchi;
Tayari Wizara ya Nishati na Madini imeshaanza kuchukua hatua ambazo zinaonesha kuwa na mwelekeo wa kutia matumaini. Naamini tutafanikiwa. Tukiwa tayari, taarifa itatolewa. Penye nia pana njia.
Napenda kutumia nafasi hii kusema mambo mawili. Kwanza, kwamba, nawapongeza viongozi wa TANESCO kwa uamuzi wao wa busara wa kuachana na nia yao ya kununua mitambo ya Dowans. Wameyasoma vizuri mazingira na nyakati na kufanya uamuzi muafaka.
Pili, niwaombe wanasiasa wenzangu kuwa, maadam waliokuwa na nia ya kununua mitambo hiyo hawanayo tena, suala hili limemalizika. Sioni sababu ya kuendelea kulumbana, kutiana vidole machoni na kutoleana maneno makali na mengine hata hayastahili kusemwa. Tumekuwa tunawatia hofu wananchi kwa jambo lisilokuwepo tena.
Nawaomba muzihifadhi nguvu zenu na bongo zenu ili muwafanyie wananchi mambo yenye tija kwao. Wanalo jukumu kubwa la kujiletea maendeleo kwa lengo la kujiondoa kwenye umaskini na kuwa na hali bora ya maisha yao. Uongozi wetu wanasiasa unahitajika sana katika juhudi zao hizo. Tuelekeze nguvu zetu na maarifa yetu huko. Wapeni pumzi wananchi kutokana na malumbano haya.
Mkutano wa G-20

Ndugu Wananchi;
Jambo la mwisho ambalo ningependa kuliongelea leo hii ni kuhusu msukusuko wa uchumi wa dunia na hasa mkutano wa Kundi la Nchi Ishirini Tajiri Duniani (G-20) ambao unategemewa kufanyika kesho tarehe 2 Aprili na kumazika tarehe 3 Aprili, 2009 mjini London, Uingereza.
Mkutano huu umeitishwa kutafuta njia za pamoja za kukabili kudorora kwa uchumi duniani. Mataifa haya tajiri ishirini, ambayo yanamiliki asilimia 85 ya uchumi wa dunia ni pamoja na Marekani, Uingereza, China, Japan, Ujerumani, Ufaransa, Afrika ya Kusini, Australia, Uturuki, Brazil, Canada, Argentina, Mexico, Indonesia, India, Italy, Urusi, Korea Kusini, Umoja wa Nchi za Ulaya na Saudi Arabia.

Ndugu Wananchi;
Uchumi wa dunia sasa hivi unapita kwenye kipindi kigumu kuliko wakati wowote katika historia ya dunia. Hali hii isipodhibitiwa kwa haraka na kwa umakini itakuwa na athari kubwa ya kushusha viwango vya hali ya maisha ya watu katika nchi zote duniani tajiri na maskini. Matajiri watakuwa maskini na maskini watakuwa fukara zaidi.
Kama nilivyosema katika hotuba zangu zilizopita, kiini cha kudorora huku kwa uchumi wa dunia ni machafuko na kuanguka kwa mfumo wa fedha wa kimataifa. Tatizo lilianzia nchini Marekani na kuenea katika mataifa tajiri ya Ulaya na Asia.

Mabenki makubwa na madogo yameanguka na kufilisika. Viwanda vikubwa na vidogo pamoja makampuni makubwa na madogo yamefilisika na kufungwa. Mamilioni ya watu wamepoteza ajira na wanaendelea kupoteza ajira.
Maelfu kwa maelfu ya watu wamepoteza nyumba zao za kuishi. Kwa ujumla, mamilioni ya watu katika mataifa tajiri wanaishi maisha ya mashaka. Wengi maisha yao yameanza kuporomoka. Nchi zetu hazihusiki na kuzuka mwa matatizo haya lakini, athari za kudorora kwa uchumi wa dunia zinatukumba sote.

Tayari tunashuhudia kupungua kwa bei na mahitaji ya bidhaa za nchi zetu kwenye soko la dunia, kupungua kwa idadi ya watalii na kupungua kwa uwekezaji na vitega uchumi kutoka nje. Aidha, mapato ya fedha za kigeni na mapato ya Serikali nayo yanapungua. Mambo haya hatimaye yatasababisha kushuka kwa uchumi wa nchi zetu, watu kupoteza ajira na kipato na hali za maisha za watu katika nchi zetu kuporomoka.

Kunahitajika hatua thabiti zichukuliwe na hatua hizo ziwahusishe na kunufaisha wadau wote. Nchi tajiri duniani zinao wajibu mkubwa zaidi. Kwanza, zina wajibu wa kuhakikisha kuwa wanadhibiti hali ili uchumi wa nchi zao usiendelee kudorora. Pia zinao wajibu wa kuzisaidia nchi kama zetu ziweze kukabiliana na athari za kudorora kwa uchumi wa dunia. Nchi tajiri zimekuwa zinachukua hatua za kunusuru uchumi wa nchi zao na bado wanaendelea. Bahati mbaya nchi zetu maskini ambazo hazina uwezo wa kuwa na mipango kama hiyo, pamoja na ukweli kwamba nazo pia zinaihitaji sana, bado hazijasaidiwa.

Ndugu Wananchi;
Mkutano wa kesho wa Mataifa 20 Tajiri Duniani umeitishwa kujadili hatua zaidi za kuchukua kuzuia mambo yasiwe mabaya zaidi na kufanya uchumi ukue. Pia wanakusudia kuzungumzia njia za kuepuka maatizo kama haya yasitokee tena duniani. Katika mkutano wa kesho pia watazungumzia namna ya kuzisaidia nchi maskini za Afrika na zile zinazoendelea ziweze kujihami na kukabiliana na athari za matatizo ya uchumi wa dunia.

Katika mkutano wao wa kwanza, uliofanyika Washington, Marekani, jambo hili halikufanyika. Wakati ule nikiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), nilimwandikia Rais George Bush wa Marekani, ambaye alikuwa Mwenyekiti wa mkutano ule, kumuomba wayaangalie maslahi ya Afrika, lakini hatukufanikiwa. Tulipata ahadi kuwa katika mkutano utakaofuata jambo hilo litazingatiwa.
Tunamshukuru Waziri Mkuu wa Uingereza, Bw. Gordon Brown kwa kutimiza ahadi yake aliyonipatia kuhusu kujali maslahi ya Afrika pamoja na kutoa fursa ya ushiriki na sauti ya Afrika kuwepo katika mkutano huu wa pili.
Kwa nia ya kupata maoni ya Waafrika hasa kuhusu matakwa na matarajio ya Afrika katika mkutano wa G-20, Waziri Mkuu wa Uingereza, tarehe 16 Machi, 2009 aliitisha mkutano maalum baina yake na viongozi kadhaa wa Afrika mjini London, Uingereza. Mkutano huo uliohusisha viongozi wa nchi za Tanzania, Liberia, Afrika Kusini, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Botswana, Misri, na Cape Verde ulikuwa na manufaa makubwa.

Ndugu Wananchi,
Nilitumia nafasi hiyo kuwasilisha maoni na mapendekezo ya mkutano wa pamoja wa Mawaziri wa Fedha, Magavana wa Benki Kuu za Afrika na Shirika la Fedha Duniani (IMF) uliofanyika hapa Dar es Salaam kuanzia tarehe 10 hadi 11 Machi, 2009.
Mapendekezo hayo yalikuwa msingi wa mazungumzo yetu katika mkutano wetu na Bw. Gordon Brown. Kwa muhtasari, matarajio ya Afrika katika mkutano wa G-20 ni kwa Afrika kusaidiwa kujikinga na kukabili madhara ya kudorora kwa uchumi wa dunia.

Miongoni mwa mambo ambayo tuliyasisitiza ni haja ya kuanzishwa mfuko maalum ambapo fedha zake zitatumika kuzisaidia nchi za Afrika kuchukua hatua za kunusuru uchumi wao kama wafanyavyo mataifa tajiri.Kwa maneno mengine tuliunga mkono pendekezo la Benki ya Dunia na kutaka Mkutano wa G-20 ukubali kwamba asilimia 0.7 ya fedha walizotumia kugharamia mipango yao ya kuchochea uchumi wao (stimulus packages) zitengwe kwa ajili ya kusaidia kuchochea kukua kwa uchumi kwa nchi za Afrika.

Pili,
tulisitiza kuwa nchi tajiri zisipunguze misaada ya maendeleo kwa nchi maskini. Badala yake misaada hiyo iongezwe kama walivyoahidi kwenye mikutano ya Monterrey, Gleneagles na kwingineko.

Tatu,
tulisema kwamba tunatarajia pia misaada kwa Afrika, na uwekezaji kutoka nje vitaelekezwa katika kujenga na kuboresha miundombinu, kuleta mapinduzi katika kilimo, kukuza biashara miongoni mwa nchi za Kiafrika na baina yake na nchi nyingine za dunia na kusaidia zaidi makundi katika jamii ambayo yanahitaji msaada zaidi (vulnerable groups).

Nne,
kwamba nchi tajiri duniani pamoja na Taasisi za Kimataifa za Fedha Duniani zilegeze masharti na kupunguza urasimu wa kupata fedha za misaada na mikopo kwa kutambua kwamba hiki ni kipindi kugumu na cha dharura. Aidha, masharti ya kukopa kutoka vyombo vingine vya fedha yalegezwe pia.

Tano,
kwamba nchi tajiri zisaidie nchi za Afrika kujenga mitaji ya vyombo vya fedha vya kikanda kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika. Na, la sita, kwamba, nchi tajiri zitakubaliana kuruhusu uwazi katika mabenki yao na taasisi zao za fedha ili kuwezesha nchi za Kiafrika kufuatilia na kurudishiwa fedha, majumba na rasilimali zilizoporwa kutoka katika bara letu na kuhifadhiwa kisirisiri katika mabenki ya nchi tajiri.

Ndugu Wananchi,
Tunamshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu Gordon Brown kwa kuyapokea mapendekezo haya ya Afrika kwa moyo mkunjufu na kuahidi kuyafikisha na kusaidia kuyatetea katika kikao hicho. Pia tunamshukuru amepokea rai ya Afrika ya kuwakilishwa kwenye mkutano huo kwa kumwalika Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Meles Zenawi, ambaye atatuwakilisha kwa kofia yake ya Uenyekiti wa NEPAD.

Ndugu Wananchi;
Mkutano huu wa G-20 ni muhimu sana kwani unalo jukumu la kihistoria la kuuokoa uchumi wa dunia. Kwa msemo wa Kiswahili tungeweza kusema kuwa kazi ya mkutano huu ni ya kufa na kupona. Mkutano ukifanikiwa, sote tumenusurika. Ukishindwa sote tutakuwa mashakani na tunaweza kuangamia. Tuwatakie viongozi wa G-20 heri na fanaka tele katika mazungumzo yao. Hatima ya maisha na ustawi wa dunia na watu wake uko mikononi mwao.

Mwisho
Ndugu Wananchi;
Mwisho kabisa napenda kuelezea masikitiko yangu kwa ajali tatu zilizotokea hivi majuzi. Ya kwanza, ni ile ajali ya magari iliyotokea mkoani Mbeya. Ya pili, ni ile ya treni mbili zilizogongana mkoani Dodoma. Na ya tatu ni ajali ya mgodi kufukia wachimbaji, wilayani Geita. Kwa ajali zote hizo tatu, moyo wangu uko pamoja na familia za wafiwa na waliojeruhiwa. Majonzi yao ndio majonzi yangu. Na machungu yao ndio machungu yangu.

Tuzidi kumuomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu wetu hao mahali pema peponi. Amin! Aidha, tunawaombea majeruhi waweze kupona haraka na kuendelea na juhudi zao za ujenzi wa Taifa. Kuhusu ajali ya treni, tutachukua hatua za kisheria kwa wote waliosababisha ajali hiyo.

Tayari wahusika, wakiwemo dereva wa treni ya mizigo, Mastesheni Masta na askari wawili waliokuwa kwenye treni ya mizigo wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za uzembe na kusababisha mauaji. Aidha, Serikali imeunda Tume ya kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.
Kwa upande wa ajali ya mgodi, napenda kuwahakikishia kuwa Serikali itafanya kila tuwezalo kusaidia juhudi za uokoaji. Ni kwa nia hiyo, nimeagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania kusaidia juhudi hizo, na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. William Ngeleja, yupo Geita kwa ajili hiyo.
Naomba nimalize kwa kuwashukuru na kuwapongeza wananchi na viongozi wote walioshiriki, na wanaoendelea kushiriki, kwa hali na mali katika juhudi za uokoaji.Mungu Ibariki AfrikaMungu Ibariki TanzaniaAsanteni sana kwa kunisikiliza!

msomaji,
Tanzania.

MELI YAKWAMA KWENYE BANDARI YA SALAMA

Hii ndio meli iliyokwama bandari pale Dar es salaam baada ya kupoteza mwelekeo. Meli hii inaitwa MSC Federica.
Jinsi Meli ilivyokwama kwenye mchanga.
Katibu Mkuu wa wizara ya Miundombinu Omar Chambo akiongea na waandishi wa habari kuhusu kukwama kwa meli hiyo ya mizigo katika eneo la Feri ya Kigamboni baada ya kutokea matatizo kwenye usukani na kushindwa kukata kona, meli ilikuwa inatokea katika Bandari ya Dar es Salaam kuelekea nchi za nje. Juhudi za kuikwamua zinaendelea ikiwa ni pamoja na kupunguza maji na mafuta kwenye meli ili kupunguza uzito
Katibu Mkuu akiangalia meli hiyo ya MSC Federica katika eneo la Feri ya Kigamboni Habour Master nahodha Juma Saire akimuonyesha Katibu Mkuu wa wizara ya Miundombinu Omar Chambo (katikati) meli hiyo ya MSC Federica iliyokwama bandalini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa bandari Ephraim Mgawe.
MSC Federica kwa mbali kutokea maeneo ya Feri ya Kigamboni . Juhudi za kuikwamua zinaendelea ikiwa ni pamoja na kupunguza maji na mafuta kwenye meli ili kupunguza uzito.

Msomaji
Dar es salaam

MACHINGA COMPLEX KATIKA HATUA ZA MWISHO

Machinga Complex jinsi inavyoonekana kwa karibu, sehemu hii ina eneo kubwa la kuegesha magari na kwa ujumla ni safi na ya kuvutia. Tuombe Mungu sehemu hii itunzwe vizuri isijegeuzwa kuwa kama sehemu ya kuuza mkaa (makaa).
Jengo hili la Machinga litakuwa na jumla ya vibanda 1,500 ambavyo kila kibanda kimoja kitagawiwa wamachinga 6. Pichani ni kibanda mojawapo ambacho kitamiliwa na wamachinga sita. Walio ndani ya kibanda hichi sio wamachinga bali wanaonyesha mfano wa jinsi mambo yatakavyokuwa biashara kitakapoanza.
Msomaji
Dar es salaam

SIKU MH CHENGE ALIPOTA AJALI MBAYA NA KUUA WATU WAWILI.

Mbunge wa CCM wa jimbo la Bariadi Mashariki , Mh, Andrew Chenge alipata ajali ya gari alilokuwa akiendesha aina ya Totota Hillux lenye namba za usajili T512ACE katika maeneo ya makutano ya barabara za Haillesalasie na Karume eneo la Oysterbay jijini na kuua watu wawili papoapo.
Gari la Mh Chenge liligonga Bajaji yenye namba za usajili T736AHC na kusababisha vifo vya watu wawili ambao walikuwa abiria katika bajaj hiyo.
Chenge akiwa Polisi Oysterbay.
Mh Chenge akiwa katika eneo la ajali.
Askari Polisi wa traffic akibeba baadhi ya mabaki yaliochwa kwenye ajali.
Mh Chenge akiwapungia watoto wa shule mkono kana kwamba alienda kufanya ziara.
Hata baadhi ya maafande pia walianza kupungia mikono watoto.
Msomaji
Dar es salaam

MKUTANO WA WADAU WA KUKUSANYA MAONI KUHUSU GHARAMA ZA USAFIRISHAJI WA MIZIGO NCHINI KWA KUTUMIA MALORI

Mkurugenzi wa sumatra Israel Sekirasa kutoka kulia akiongea jambo kuhusianana Mkutano wa wadau wa usafirishaji wa mizigo kwa kutumia Malori hapa nchini katika ni Makamu Mwenyekiti wa Mkutano huo Willy Kishimbo na Makamo Mwenyekii wa Tatoa Alkarlim Daud.

Mkutano huo ulio wahusisha wadau wa usafirishaji na wamiliki wa malori ulilenga maboresho ya usafirishaji ambapo baadhi wafanyashughuli hiyo wamekuwa wakilalamika kuwa gharama ya usaafirishaji mizigo imekuwa ikipanda zaidi. Hivi karibuni Waziri MKUU Mizengo Kayanda Pinda alitembeleas katika masoko yote ya jiji la Dar es Salaam na kujionea shughuli za masoka ambapo alipofika katika soko kuu la kariakaoo,aliambiwa na Mkuu wa soko la kariakoo kuwa kwa sasa Magari makubwa yamizigo hayaluhusiwi kuingia katika soko hilo, hata hivyo kiongozi huyo alitabainisha kuwa mbona magari ya soda na yale yanayosambaza vinywaji aina ya pombe yanaingia katika maeneo hayo ya soko na hayatozwi ushuru mkubwa na hayakamatwi.

Msomaji
Dar es salaam

WAZIRI MAGEMBE ALIPOTANGAZA WALIOFAURU KUINGIA KIDATO CHA TANO 2009

Waziri wa Elimu na Mafunzo Prof. Jumanne Maghembe (katikati) akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa wanafunzi wa kuingia kidato cha tano na katika vyuo vya ufundi kwa mwaka wa masomo 2009. Kushoto ni Kaimu Kamishina wa Elimu Leonard Musaroche na kulia ni Msaidizi wa Waziri Alfred Kilasi.

Msomaji
Dar es salaam

MTAMBO WA SONGAS KUANZA UZALISHAJI NDANI YA MAJUMA MAWILI

Waziri ngeleja akiongea na wana habari katika moja ya mikutano yake.
Serikali imesema kuwa ndani ya wiki moja kuanzia tarehe 28/03/2009 mtambo wa kuzalisha umeme wa Kampuni ya Songas ulioharibika utakuwa tayari na kuanza kufanya kazi kama kawaida.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alipofanya ziara ya kutembelea mitambo hiyo iliyopo Ubungo jijini Dar es Salaam ili kuona maendeleo ya matengenezo ya mitambo miwili iliyosababisha upungufu wa megawati 50 za umeme katika gridi ya Taifa.

“Kwa taratibu za kawaida matengenezo ya mtambo huu yangechukua miezi mitatu hadi minne ila mafundi wanafanya kazi ya matengenezo kwa bidii na hatua waliyofikia watachukua muda mfupi kumaliza kazi hii”, alisema waziri Ngelleja.

Aliendelea kusema kuwa mgao unaoendelea ni kutokana na ajali ya kuharibika kwa mtambo mmoja kwani mtambo mwingine uko katika matengenezo ya kawaida ila baada ya kuharibika kwa mtambo huo ndiyo tatizo limeongezeka zaidi.

Ngelleja alisema kuwa, “Serikali haina mpango wa kuwafanya wananchi waishi gizani zipo hatua nyingi ambazo wanazichukua na watazitolea ufafanuzi kadri siku zinavyokwenda”.

Mtambo wa pili wenye uwezo wa kuzalisha megawati 35 ambao uko katika matengenezo ya kawaida unatarajia kuanza kazi baada ya wiki mbili tangu kuanza kwa matengenezo hayo.

Hivi sasa mtambo ulioharibika umefumuliwa na kuanza kutengenezwa upya na una uwezo wa kuzalisha megawati 20 za umeme kama utaanza kazi utakuwa umepunguza makali ya mgao wa umeme kwa kiasi fulani.

Kuanzia Alhamisi wiki hii jijini Dar es Salaam kumeanza mgao wa umeme ambao unaleta usumbufu kwa wananchi hii ni kutokana na kuharibika kwa mitambo hiyo .

Msomaji
Dar es salaam

Wednesday, April 1, 2009

Baadhi ya wanajeshi wanaokwenda Darful - Sudan kulinda amani wakiwa katika picha ya pamoja leo. wanajeshi hao waliagwa na katibu mkuu mstaafu wa African Union Organisation (OAU) Dk. Salim Ahmed Salim leo.

Msomaji,
Tanzania.
Katibu mkuu mstaafu wa iliyokuwa African Organization Union (OAU) ambayo kwa sasa ni African Union (AU) Dk. Salim Ahmed Salim akizungumza na waandishi wa habari mara baada kuwaaga wanajeshi wanaokwenda kulinda amani huko Darful - Sudan.
msomaji,
Tanzania.
Waziri wa mkuu wa Australia akizungumza na makamu wa rais wa mazingira Dk. Batilda Burian
kwenye Hotel ya Kempinsk jijini Dar es salaam leo asubuhi, Dk. Batilda alifika kumuaga waziri mkuu huyo akiambatana na mwanae bi. Shymaa.

msomaji
Tanzania.