Monday, April 26, 2010

MAADHIMISHO YA MIAKA 46 YA MUUNGANO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akipungia mkono wananchi mbalimbali waliojitokeza kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam ambapo wakazi mbalimbali walijitokeza katika sherehe hizo, kulia ni mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.
Viongozi wa vyama mbalimbali pamoja na maafisa kutoka serikalini nao walikuwepo katika maadhimisho hayo.
Wageni waalikwa mbalimbali na mabalozi wakifuatilia kwa karibu kila kilichokuwa kikendelea kwenye uwanja wa Uhuru leo jijini Dar es salaam.
Wanafunzi wa shule mbalimbali jijini Dar es salaam wakicheza halaiki wakati wa maadhimisho ya miaka 46 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Uhuru leo.

Msomaji
Dar es salaam

No comments: