Thursday, April 22, 2010

Matukio Bungeni Dodoma Leo

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mwantumu Mahiza (mwenyemiwani) akiwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) leo wakati wanafunzi hao walipokwenda kuangalia maeneo mbalimbali ya shughuli za Bunge mjini Dodoma leo. Mwenyekiti wa Kamati za Mahesabu za Mashirika ya Umma Zitto Kabwe leo Bungeni akitoa taarifa ya Kamati za Hesabu za Mashirika ya Umma pamoja na mapendekezo na maoni yaliyomo kwenye taarifa . Picha na Mwanakombo Jumaa.
Mbunge wa Mtera Johhn Malecela Akichangia sheria ya Malisho na vyakula vya mifugo
Mbunge wa Monduli Edward Lowassa (kulia) akimsikiliza Mbunge wa Kiteto Benedict Nangoro (kushoto) leo ndani ya Ukumbi wa Bunge -Dodoma. Picha na Mwanakombo Jumaa
waziri wa Madini na Nishati William Ngeleja (kulia) na Naibu Waziri wa Madini na Nishati Adam Malima wakizungumza leo katika viwanja vya Bunge Dodoma baada ya Waziri Ngeleja kuwasilisha Muswada wa Sheria ya Madini wa Mwaka 2010.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza Wa Rais (Muungano) Muhammed Seif Khatib (kushoto) akizungumza na waandishi wa Habari Dododma leo kuhusu mambo mbalimbali ya Muungano. Mwengine ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano.
Msomaji
Dodoma

No comments: