Monday, April 12, 2010

UCHAGUZI 2010!!

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akibonyeza kitufe kwenye kompyuta ndogo kuashiria uzinduzi wa uchangiaji kupitia simu za mikononi (CCM Mobile System) Dar es Salaam juzi usiku. Mfumo huo utawawezesha wanachama na wapenzi wa chama hicho kukichangia fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao baadaye mwezi Oktoba kwa kujiunga na namba 15016. Kwa mujibu wa Kikwete, chama kimepanga kukusanya shilingi bilioni 40 kufanikisha uchaguzi mkuu. Anayeshuhudia ni Katibu Mkuu wa CCM-Taifa, Yusuf Makamba.

No comments: