Friday, April 23, 2010

Viongozi wa Tanzania na Msumbiji wakagua maadalizi ya uzinduzi wa daraja la umoja

Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu Omari Chambo akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi za Jamii na Maendeleo ya Makazi wa Msumbiji Bi. Maria Luisa Mathe(mwenye shati jeupe) na Mkuu wa wilaya ya Nanyumbu Bi. Fatma Salum Ally wakielekea sehemu ya juu ya Daraja la Umoja kukagua maandalizi ya sherehe za Uzinduzi wa Daraja hilo tarehe 12 mwezi ujao jana katika eneo la Mtambaswala wilayani Nanyumbu mpakani mwa Tanzania na Msumbiji
Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu Omari Chambo (katikati) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi za Jamii na Maendeleo ya Makazi wa Msumbiji (Mwenye shati jeupe) Bi. Maria Luisa Mathe na Mkuu wa wilaya ya Nanyumbu Bi. Fatma Salum Ally(kushoto) wakikagua Daraja la Umoja eneo la Mtambaswala mpakani mwa Tanzania na Msumbiji katika maandalizi ya sherehe za Uzinduzi wa Daraja hilo mwezi ujao.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu Omari Chambo akiwaongoza viongozi mbalimbali kutoka wilayani Nanyumbu na Msumbiji kukagua maandalizi ya sherehe za uzinduzi wa daraja hilo katika eneo la chini ya Daraja la Umoja lililojengwa kwa Ushirikiano kati ya Tanzania na Msumbiji katika eneo la Mtambaswala wilayani Nanyumbu jana.

Msomaji
Nanyumbu

No comments: