Msomaji
Dar es salaam
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja akikabidhi kwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete mchango wa jumla ya Tshs.1,482,200/- kutoka kwa jumuiya ya umoja wa vijana mkoa wa Shinyanga kwaajili ya fomu ya ugombea urais ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete.Makabidhiano hayo yalifanyika jana jioni ikulu jijini Dar es Salaam na kushudiwa na viongozi wote wa CCM mkoa wa Shinyanga.Kulia ni Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Shinyanga Stephen Julius Masele amnaye pia alisoma ujumbe maalumu wa vijana wa mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete, katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba(katikati) na makamu mwenyekiti CCM Bara Pius Msekwa(kulia) wakituma ujumbe mfupi sms kupitia simu zao ili kuchangia CCM wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia CCM kupitia simu za mikononi ulifanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akibonyeza kitufe kwenye kompyuta ndogo kuashiria uzinduzi wa uchangiaji kupitia simu za mikononi (CCM Mobile System) Dar es Salaam juzi usiku. Mfumo huo utawawezesha wanachama na wapenzi wa chama hicho kukichangia fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao baadaye mwezi Oktoba kwa kujiunga na namba 15016. Kwa mujibu wa Kikwete, chama kimepanga kukusanya shilingi bilioni 40 kufanikisha uchaguzi mkuu. Anayeshuhudia ni Katibu Mkuu wa CCM-Taifa, Yusuf Makamba.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete(Watano kulia) Rais Wa Zanzibar Amani Abeid Karume (Wasita kulia),pamoja viongozi wengine wa kitaifa wakiomba dua katika kaburi la muasisi wa mapinduzi ya Zanzibar Hayati Mzee Abeid Amani Karume huko katika ofisi kuu ya CCm Kisiwandui Zanzibar leo asubuhi.wengine katika picha kutoka kushoto Naibu Waziri kiongozi wa SMZ Ali Juma Shamuhuna,Naibu Katibu mkuu CCM Zanzibar Salehe Ramadhani Feruzi,Waziri kiongozi wa SMZ Shamsi Vuai Nahodha, na makamu wa Rais Dr.Ali Mohamed Shein.
Maghorofa mpya yaliyopo mtaa wa Michenzani Zanzibar yaliyoanza kujengwa kwaajili ya makazi bora ya Wananchi wa Zanzibar na hayati Mzee Abeid Amani Karume na kukamilishwa na Rais wa sasa Amani Abeid Karume.Makazi hayo tayari yamenza kugawanywa kwa wananchi waliokusudiwa kwa utaratibu maalumu 
Rais Jakaya mrisho Kikwete, Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar(kulia) na Mwenyekiti wa jumuiya ya umojawa Vijana wa CCM Bwana Yusuf Masauni wakati wa mapokezi ya maandamano ya umoja wa vijana wa CCM mjini Zanzibar jana jioni.
Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mwenyekiti wa Jumuiya ya umoja wa Vijana CCM Yusuf Masauni(wapili kushoto), Makamu mwenyekiti wa jumuiya hiyo Bwana Beno Malisa(kushoto), na katibu mkuu wa jumuiya ya umoja wa Vijana CCM Bwana Martin Shigela wakiyapokea maandamano ya vijana wa CCM katika viwanja vya CCM Maisara Zanzibar jana jioni.Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye aliyekuwa mgeni Rasmi katika maandamano hayo aliwahutubia vijana hao.
Baadhi ya vijana wananchama wa UVCCM wakishangilia hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyoitoa wakati wa kilele cha maandamano yaliyoandaliwa na jumuiya hiyo mjini Zanzibar kumuenzi muasisi wa mapinduzi ya zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume.