Sunday, September 20, 2009

Rais kikwete ameondoka nchini leo kuelekea Marekani kuhudhuria kikao cha 64 cha UN

RAIS Jakaya Kikwete ameondoka nchini leo jioni kwenda New York, Marekani kuhudhuria kikao cha 64 cha Baraza la Umoja wa Mataifa (UN) ambalo atalihutubia Alhamisi ijayo.
Mbali na kuhudhuria baraza hilo litakalofunguliwa rasmi Jumatano, Rais Kikwete anatarajiwa kuhudhuria mikutano mbalimbali iliyoandaliwa na UN kwa ajili ya viongozi wakuu wa nchi watakaokuwepo nchini humo.

Baadhi ya mikutano ni pamoja na unaohusu mabadiliko ya hali ya hewa unaoandaliwa na Katibu Mkuu wa UN, Ban Ki Moon.

Taarifa ya Ikulu pia imesema Rais atahudhuria kikao cha uzinduzi wa mpango wa pamoja wa viongozi wa Afrika kupambana na malaria Afrika ambao Tanzania ni mwenyekiti mweza na imeshirikiana na umoja huo kuuandaa.

Katika kikao kingine, Kikwete pamoja na Waziri Mkuu wa Uingereza, Gordon Brown kwa pamoja wataongoza kikao cha viongozi kuzungumzia malengo ya milennia namba 4 na 5, malengo yanayohusu kupunguza vifo vya watoto wachanga na wajawazito

No comments: