Tuesday, September 15, 2009

Mafunzo ya Wiki Mbili Kwa Makatibu Wakuu Yalivyofunguliwa

Katibu Mkuu kiongozi Philemon Luhanjo akiongea na waandishi wa habari kuhusu mafunzo ya uongozi yanayofanyika katika hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam.Mafunzo hayo ya wiki mbili ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma yanatolewa kwa Makatibu wakuu, Manaibu Katibu wakuu pamoja wakurugenzi walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa hizo.Picha Zote na Anna Nkinda - Maelezo
Washiriki wa mafunzo ya uongozi kwa Makatibu wakuu,Manaibu Katibu wakuu pamoja na wakurugenzi walioteuliwa hivi karibuni kushika nyadhifa hizo wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufunguliwa kwa mafunzo hayo ya wiki mbili.Waliokaa mstari wa mbele katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo kulia kwake ni Katibu Mkuu Utumishi George Yambesi na kushoto kwake ni John Odebiy ambaye ni Mwezeshaji wa mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Msomaji
Dar es salaam

No comments: