Wednesday, September 16, 2009

Msimamo wa Spika Samueli Sitta Safi-Mwakilishi UNDP..

Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Samuel Sitta,ambaye amepewa sifa kwa kutetea maslahi ya nchi kwa njia ya kidemokrasia akiingia bungeni.


Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alain Noudehou, amepongeza msimamo wa spika wa Bunge,Samuel Sitta bungeni,akisema unawakilisha demokrasia ya kweli katika kutetea maslahi ya wananchi.
Noudehou alisema hayo jana alipokuwa akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya demokrasia iliyoandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania(TCD)na kufanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

“Pamoja na mambo mengine alisema Mh. Spika wa bunge amefanikiwa kukamilisha Mpango wa Maendeleo ya Bunge ambao umetoa picha kamili ya Bunge madhubuti linalowajibika kwa watu wake. UNDP iko tayari kumsaidia kutekeleza mkakati huo,”alisema Noudehou.

Kwa mujibu wa Noudehou kama Tanzania inataka kuendelea kujimarisha kidemokrasia, haina budi kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na changamoto zinazohusu uwajibikaji, uwakilishi na usawa.

“Hali hiyo itawezesha kujenga jamii ambayo itajihakikishia maendeleo ya watu,kupatikana kwa haki na ukombozi wa kiraia kwa Watanzania wote,alisema.Aliongeza kuwa ili Tanzania iweze kukabiliana na changamoto hizo inahitaji kuegemea kwenye kuimarisha asasi za kidemokrasia katika kuunga mkono chaguzi,kulinda utawala wa sheria na kuhamasisha mazungumzo ya ndani ya vyama vya siasa.

“Kuimarisha uwezo wa taasisi za kidemokrasia kama Bunge,Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa(Takukuru),vyombo vya usimamizi wa chaguzi na kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari kutaendelea kuleta mabadiliko ya kidemokrasia,” alifafanua.“Haya mazungumzo ya vyama vya siasa kwa sasa ni muhimu sana kwa Tanzania katika kipindi hiki cha kuingia kwenye uchaguzi.Mazungumzo hayo yanapanua utamaduni na uvumilivu wa kisiasa.”

Msomaji
Dar es salaam

No comments: