Thursday, July 8, 2010

Bi Zainab Janguo kuwakilisha CCM Marekani huko Dodoma

Katibu wa uenezi na siasa wa CCM tawi la Marekani Bi. Zainab Janguo ameondoka hapa nchini kuelekea mjini Dodoma kuhudhuria mkutano mkuu wa 9 wa CCM unaotarajiwa kuanza hapo Julai 10 na 11 mjini humo. Mwakilishi huyo wa CCM tawi la Marekani ameondoka hapa kufuatia mwaliko wa kuhudhuria mkutano huo katika barua iliyotumwa na kusainiwa na Katibu Mkuu wa CCM Mh. Yusuf R. Makamba.
Bi Janguo pia anatarajiwa kuanza ziara ya kimafunzo kwa vitendo katika idara mbalimbali za chama kwa muda wa wiki tatu baada ya kumalizika kwa mkutano mkuu huo. CCM tawi la Marekani linamtakia mwakilishi wetu safari na uwakilishi mwema katika mkutano huo.

No comments: