RAIS JAKAYA KIKWETE AKIZINDUA KIVUKO CHA MV MAGOGONI
Hiki ndiyo kivuko cha MV Magogoni kilichozinduliwa leo na Rais jakaya Mrisho Kikwete
Rais jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kama ishara ya kuzindua kivuko cha MV Magogoni Tayari kwa kuanza Rasmi kazi ya kuvusha abiria na mizigo kati ya Kigamboni na Posta, Kivuko hicho kilianza kujengwa mwaka 2007 na kilikamilika mwaka 2008 kina uwezo wa kubeba tani 500, ujenzi wake umegharimu jumla ya shilingi za kitanzania bilioni 8.3 huku kikiwa na Uwezo wa kuchukua watu 2000 na magari 60, katika picha kushoto ni Waziri wa Wizara ya Miundombinu Mh. Shukuru Kawambwa na kulia ni Mkuu wa mkoa wa Dar es alaam William Lukuvi na anayefuata ni Naibu Waziri wa Wizara ya Miundombinu Ezekiel Chiburunje Uzinduzi huo umefanyika leo asubuhi eneo la Ferri.
Rais Jakaya Kikwete akishuka kutoka ndani ya Kivuko mara baada ya kukizindua rasmi huku akiongozwa na wasaidizi wake, kulia ni Waziri wa Ardhi na Makazi Mh. John Chiligati na Nyuma ya Rais jakaya kushoto ni Waziri wa Miundombinu Mh. Shukuru kawambwawananchi wa mkoa wa Dar es alaam wakiwa wamekusanyika eneo la Kigamboni tayari kwa kumpokea Mh. Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuzindua kivuko cha MV. Magogoni leo.
Kap. John Komba na kundi zima la TOT wakitumbuiza kwa nyimbo za kwaya kabla ya mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete kuwasili eneo la Ferri Kigamboni tayari kwa kuzindua Kivuko cha MV Magogoni leo asubuhi.
Imani za CCM zimejengwa chini ya misingi ya usawa kwani binadamu wote ni sawa. CCM kinalenga kumuwezesha mwananchi yeyote wa Tanzania kupata maendeleo.
U.S.A.
Contact
Welcome to the blog of CCM members living in the State of Texas in the United States of America. If you'd like more information about CCM, please contact us at ccmtexas12@gmail.com. We welcome suggestions and comments. If you'd like to become a member, email us and we'll assist you as quickly as possible.
What's the most pressing issue for Tanzanians abroad?
No comments:
Post a Comment