WAHANGA WA MABOMU WAANDAMANA NA MABANGO, WAMTAKA WAZIRI MKUU!!
Wakazi wa Mbagala kuu wakiandamana na mabango yao baada ya kutoridhishwa na ugawaji wa vifaa hivyo kwa wahanga wa mabomu, kutokana na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa katika eneo hilo kushindwa kushirikiana vizuri katika kusimamia zoezi hilo, wakazi hao wamesema katika hali isiyo ya kawaida kuna hata baadhi ya viongozi wa kitaifa wa wametembelea eneo hilo na kugeuza ni sehemu ya kampeni, badala ya kusaidia wananchi wenye matatizo kwa wakati huu, katika eneo hilo wajumbe wengi wa nyumba kumi wanatoka chama cha CUF wakati Diwani wa kata hiyo anatoka CCM hivyo wakazi hao wanasema ushirikiano umekuwa mdogo kutokana na kila mtu anavutia kwake lakini sisi wananchi tunahitaji huduma kwa sasa hiyo siasa haitusaidii kwa kipindi hiki zaidi ya kutuumiza tu ukizingatia kuwa mvua inanyesha kwa wingi
No comments:
Post a Comment